Page 111 - Historiayatznamaadili
P. 111

Licha ya shughuli za kuzalisha mali, jamii zilishirikiana katika
              masuala ya jamii kama vile sherehe, majanga na michezo. Watu
              walishiriki kwa kukaa pamoja, kula, kuimba na kucheza. Ushiriki
              huu ulisaidia kujenga uhusiano mwema katika jamii za kale.
          FOR ONLINE READING ONLY

                      Zoezi namba 2

                1.  Eleza mambo uliyojifunza kutokana na ushirikiano na
                      uhusiano wa jamii wakati wa mfumo wa ujima.

                2.  Eleza tofauti ya ushirikiano na uhusiano uliokuwapo
                      katika jamii enzi za ujima na sasa.





              Ushirikiano na uhusiano wa kijamii katika misingi ya ukabaila


              Kadiri maendeleo ya jamii yalivyokua ndivyo ushirikiano na
              uhusiano katika jamii ulivyobadilika. Pamoja na jamii za kale
              kuendelea kushirikiana katika mambo mbalimbali, taratibu
              misingi ya ushirikiano na uhusiano ilianza kubadilika. Mfano,

              ugunduzi wa zana za chuma, ulileta mabadiliko katika mfumo
              wa maisha ya binadamu. Ugunduzi wa chuma uliwezesha watu
              kulima eneo kubwa zaidi na kuwa na ziada. Hivyo, baadhi ya
              watu walianza kumiliki maeneo makubwa zaidi ya watu wengine.

              Huu ukawa ndio mwanzo wa matabaka katika jamii na kuanza
              kuvunjika kwa misingi ya ushirikiano na uhusiano uliyojengwa
              katika ujima. Matabaka ya watawala na watawaliwa yalianza
              kukua. Tabaka la watawala lilikuwa na mali, kwani walimiliki

              ardhi kubwa. Tabaka tawaliwa halikuwa na umiliki wa ardhi.
              Tabaka la waliojilimbikizia ardhi lilianza kunyonya watu wengine
              kwa kuwapa maeneo ya mashamba na mifugo, kisha kudai fidia
              kama ushuru. Huu ukawa mwanzo wa mfumo wa ushirikiano na

              uhusiano wenye msingi ya kiunyonyaji katika jamii uliojulikana
              kama “ukabaila”.





                                                   104




                                                                                          06/11/2024   11:30:17
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   104
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   104                                    06/11/2024   11:30:17
   106   107   108   109   110   111   112   113   114   115   116