Page 110 - Historiayatznamaadili
P. 110

FOR ONLINE READING ONLY

























                        Kielelezo namba 1: Zana za mawe zilizowekwa mpini


              Watu wote walifanya kazi pamoja katika kipindi cha ujima. Mfano
              katika shughuli za uwindaji, waliwinda pamoja na mawindo
              yaliyopatikana waligawana kwa usawa. Aina hii ya ushirikiano

              na uhusiano iliondoa mianya ya unyonyaji, ubaguzi na dhuluma
              kutokana na kuwapo kwa usawa katika umiliki na ugawaji wa
              rasilimali. Pia, kutafuta maslahi kwa pamoja kuliongeza uhusiano
              katika jamii za kale. Umiliki wa rasilimali katika jamii kama mifugo

              na ardhi ulikuwa wa pamoja na siyo wa binafsi. Hii iliondoa
              matabaka, ya wale wenye nacho kwa wingi na wasiokuwa nacho.
              Watu wote walikuwa sawa. Mgawanyo wa kazi wakati wa ujima
              ulizingatia jinsi na rika. Hii ilisaidia kuweka usawa katika kazi

              kulingana na uwezo, uzoefu, umri na majukumu katika jinsi. Kila
              mtu alifanya kazi kwa kujituma na kwa bidii. Mfumo wa ujima
              ulikuwapo zaidi katika hatua za awali za maendeleo ya jamii.
              Mfumo wa ujima ulisaidia kukuza ushirikiano na uhusiano wenye

              misingi ya usawa katika jamii za kale.


                                                   103




                                                                                          06/11/2024   11:30:17
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   103
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   103                                    06/11/2024   11:30:17
   105   106   107   108   109   110   111   112   113   114   115