Page 113 - Historiayatznamaadili
P. 113

Zoezi namba 3

                1.  Eleza misingi ya ushirikiano na uhusiano wakati wa
                      ukabaila.

                2.  Je, ni mambo yapi ya kujifunza kutokana na ushirikiano
          FOR ONLINE READING ONLY
                      na uhusiano katika ukabaila?
                3.  Eleza mambo uliyojifunza kuhusu ushirikiano na uhusiano

                      wa kijamii kabla ya ukoloni.


              Ushirikiano na uhusiano katika uchumi
              Ushirikiano na uhusiano katika uchumi ulijengwa zaidi katika
              misingi ya biashara kati ya jamii moja na nyingine. Ushirikiano
              na uhusiano huu ulianza taratibu ambapo jamii moja na nyingine
              zilibadilishana bidhaa walizozalisha. Ushirikiano na uhusiano huu
              ulisababishwa na uwapo wa shughuli tofauti za uchumi, kama
              vile kilimo, ufugaji, uvuvi, uhunzi, ususi, uchongaji na kadhalika.
              Hii ilisababisha uhitaji kati ya jamii na jamii. Hivyo, jamii zilianza
              kushirikiana na kuhusiana kibiashara kwa kubadilishana bidhaa
              kwa bidhaa kati ya kaya na kaya, jamii na jamii na hatimaye na
              jamii za mbali. Kielelezo namba 2, kinaonesha watu wakifanya
              biashara za kubadilishana.






























                    Kielelezo namba 2: Watu wakibadilishana bidhaa kwa bidhaa


                                                   106




                                                                                          06/11/2024   11:30:17
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   106
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   106                                    06/11/2024   11:30:17
   108   109   110   111   112   113   114   115   116   117   118