Page 138 - Historiayatznamaadili
P. 138

Mwinyi Mkuu alikuwa mtu wa kuheshimika sana. Mwinyi alipopita
              mahali, watu wote walilazimika kupiga magoti. Pia, mtu yeyote
              aliyekuwapo juu ya paa la nyumba au juu ya mti kwa muda
              huo alilazimika kushuka mpaka Mwinyi alipopita. Wavuvi wote
          FOR ONLINE READING ONLY
              waliporudi kuvua samaki walilazimika kupeleka samaki wazuri na
              wakubwa kwa Mwinyi Mkuu. Wafugaji nao walilazimika kupeleka
              nyama ya nundu kila wachinjapo ng’ombe kwa Mwinyi. Hii ni
              kwa sababu hakuna mtu yeyote aliyeruhusiwa kula nyama ya

              nundu zaidi ya Mwinyi. Jamii hizi ziliamini kwamba nyama ya
              nundu ina mafuta mengi hivyo, ilipaswa kuliwa na mtawala.


              Utawala  huu  msingi  wake  mkubwa  ulikuwa  kumiliki  ardhi.
              Tabaka la mamwinyi pekee ndilo lililomiliki ardhi. Ardhi ya
              mamwinyi ililimwa mazao ya chakula na biashara kama vile
              mpunga  na  minazi.  Mamwinyi  waliwatumia  watumwa  na
              watwana katika kuhudumia mashamba yao. Mfano, maeneo

              ya Zanzibar yaliyokuwa chini ya himaya ya Mwinyi Mkuu ni
              Mfenesini, Ndagaa, Kikungwi, Mchangani, Chwaka, Marumbi,
              Uroa, Pongwe na Unguja Ukuu. Utawala wa Umwinyi ulisaidiwa

              na Wajumbe na Masheha. Viongozi hao walipokea maagizo
              kutoka kwa Mwinyi Mkuu na kuwapelekea wananchi kwa ajili
              ya utekelezaji.


                                Kazi ya kufanya namba 10

                           Soma matini mbalimbali kuhusu tawala za kifalme
                           na kimwinyi kabla ya ukoloni, kisha andika tofauti
                           za tawala hizo.




              Mamlaka za kirika
              Jamii zilizokuwa na mfumo wa kiutawala wa rika ni jamii za

              wafugaji, mfano Wamasai.  Mfumo wa utawala wa kirika,
              ulijulikana hivyo kwa kuwa uligawa mamlaka au madaraka
              kulingana na umri au rika. Mfano, jamii ya Wamasai ilikuwa na



                                                   131




                                                                                          06/11/2024   11:30:22
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   131                                    06/11/2024   11:30:22
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   131
   133   134   135   136   137   138   139   140   141   142   143