Page 143 - Historiayatznamaadili
P. 143

Zoezi la jumla


               1.  Eleza sababu kuu tatu (3) za kukua kwa mamlaka za
                     viongozi wa jadi kabla ya kuja kwa ukoloni nchini.
          FOR ONLINE READING ONLY
               2.  Andika neno NDIYO mbele ya sentensi ambayo ni kweli
                     na neno HAPANA mbele ya sentensi ambayo si kweli.
                       (i)  Mojawapo ya jukumu la viongozi wa jadi ni
                            kusimamia masuala ya mila na desturi za jamii
                            zao ____________

                       (ii)  Biashara za masafa marefu zilisaidia kukua kwa
                            mamlaka za viongozi wa jadi kabla ya ukoloni
                            ____________

                       (iii)  Viongozi wa jadi waliruhusu kirahisi wageni kuingia
                            katika himaya zao __________________
                       (iv) Mamlaka za kirika zilikuwa na mchango mkubwa
                            katika kuleta maendeleo ya jamii zao_____________

                       (v)  Ugunduzi wa chuma ulichangia kukua na kuimarika
                            kwa mamlaka za jadi nchini______________
               3.  Je, ni mafanikio gani yaliyosababishwa na mamlaka za
                     jadi nchini kabla ya ukoloni?

               4.  Eleza ni jinsi gani ugunduzi wa chuma ulichangia kukua
                     na kuimarika kwa mamlaka za jadi nchini.

               5.  Je, tunawezaje kuendeleza mbinu za uongozi zilizotumiwa
                     na mamlaka za jadi katika kuleta maendeleo nchini kwa
                     sasa?


              Msamiati


              Jadi             asili, kale au chanzo cha jambo fulani

              Himaya           eneo la utawala wa kiongozi mmoja, mara nyingi

                               huwa na mipaka
              Mamlaka          nguvu au uwezo aliopewa kiongozi katika eneo

                               fulani ya kiutawala na maamuzi


                                                   136




                                                                                          06/11/2024   11:30:22
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   136
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   136                                    06/11/2024   11:30:22
   138   139   140   141   142   143   144   145   146   147   148