Page 147 - Historiayatznamaadili
P. 147

(d)  Kulinda maadili ya jamii zao dhidi ya uharibifu kutoka
                    kwa wageni. Mamlaka za jadi zililinda jamii zao dhidi ya
                    mwingiliano wa maadili ya kigeni. Hivyo, zilipiga marufuku
                    mawazo, itikadi au mifumo ya maisha, mila na desturi
                    zilizokuwa tofauti na za jamii zao. Mfano, mamlaka za
          FOR ONLINE READING ONLY
                    Wangoni zilipinga mfumo wa kilimo ulioletwa na Wajerumani
                    baada ya kugundua kuwa ulikiuka maadili ya mababu zao.
                    Vita ya Majimaji chini ya Kinjekitile Ngwale, inaweza ikawa

                    na sababu nyingi, lakini sababu za msingi zilitokana na
                    Wajerumani kuvuruga maadili ya jamii za watu wa Kusini
                    mwa Tanzania. Aidha, ulinzi wa maadili ulienda sambamba
                    na kurithisha maadili ya jamii zao kutoka kizazi kimoja hadi
                    kingine.


                      Zoezi namba 1

                1.  Bainisha mchango wa mamlaka za jadi katika kukuza

                      na kutunza maadili nchini.

                2.  Eleza mambo ya kuendeleza katika kukuza na kutunza
                      maadili nchini kwa sasa.



              Mbinu zilizotumika katika ukuzaji na utunzaji wa maadili

              Mamlaka za jadi zilitumia mbinu mbalimbali katika kukuza na
              kutunza maadili ya jamii kama vile:


              (a)  Ibada za kijadi. Ibada zilizoambatana na matambiko
                    zilifanyika ili kuomba nguvu za miungu, malaika na mizimu ya
                    jamii kusimamia maadili. Jamii iliamini iwapo mtu angekiuka
                    maadili na ibada za matambiko zingefanyika, angeweza
                    kupata laana na kukumbwa na majanga. Mfano, mhusika
                    kuwa mwehu, kutokuzaa, kukosa mafanikio katika maisha,
                    kupata ugonjwa usiotibika na kadhalika. Hii ilisababisha
                    jamii kuzitii mamlaka za jadi katika usimamizi wa maadili

                    ya jamii kwani zilisimamia miungu ya jamii.




                                                   140




                                                                                          06/11/2024   11:30:23
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   140                                    06/11/2024   11:30:23
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   140
   142   143   144   145   146   147   148   149   150   151   152