Page 142 - Historiayatznamaadili
P. 142

Mafanikio yaliyopatikana kutokana na mfumo wa uongozi
              wa jadi
              Viongozi wa jadi walisababisha maendeleo makubwa katika

              tawala zao. Yafuatayo ni baadhi ya mafanikio ya tawala za jadi
          FOR ONLINE READING ONLY
              kabla ya ukoloni:

                 (a)  Kupanuka na kuimarika kwa mamlaka za jadi katika jamii
                       zao kama vile za Wafalme, Watemi, Machifu, Mangi na
                       kadhalika. Mamlaka hizo zilisaidia wakati wa harakati za
                       kudai uhuru;

                 (b)  Kuwaunganisha watu, hivyo, kuwa na umoja, heshima

                       na ushirikiano kati ya wanajamii;
                 (c)  Kupambana na wavamizi wa ukoloni katika maeneo

                       yao, hivyo, kujenga chachu ya kupinga ukoloni nchini;

                 (d)  Kutatua na kuondoa migogoro ndani ya jamii na kuleta
                       amani, utulivu na ustawi wa jamii;

                 (e)  Kujenga misingi ya kupenda kazi katika jamii;

                 (f)  Kuimarisha na kukuza shughuli za uchumi katika jamii,
                       hivyo watu kuzalisha kwa matumizi binafsi na ziada;

                 (g)  Kupanuka kwa ujenzi wa makazi;

                 (h)  Kuondoa migogoro ya ardhi kwa kuweka utaratibu mzuri
                       wa matumizi ya ardhi;

                 (i)  Kulinda utamaduni wa jamii; na

                 (j)  Kuimarisha mgawanyo na usimamizi mzuri wa kazi.


                                Kazi ya kufanya namba 13


                           Soma matini kuhusu utawala wa jadi, kisha andika
                           taarifa fupi kuhusu viongozi watano (5) wa jadi
                           ambao hawakutajwa katika sura hii.







                                                   135




                                                                                          06/11/2024   11:30:22
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   135                                    06/11/2024   11:30:22
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   135
   137   138   139   140   141   142   143   144   145   146   147