Page 145 - Historiayatznamaadili
P. 145

inafuata maadili ya jamii husika. Hii ilisaidia jamii kufuata maadili
              yaliyokubalika na jamii nzima. Aidha, mifumo hii ilishirikiana na
              kutegemeana katika kukuza na kutunza maadili.


                                Kazi ya kufanya namba 2
          FOR ONLINE READING ONLY
                           Jadili namna mamlaka za jadi zinavyosimamia
                           ukuzaji na utunzaji wa maadili katika ukoo.





              Mamlaka za jadi

              Jamii zilikuwa na koo mbalimbali, ambazo zilikuwa chini ya
              mamlaka za jadi. Mamlaka za jadi zilikuwa na viongozi wakuu,

              ambao walijulikana kama Machifu, Watemi, Mutwa Mangi au
              Wafalme (Omukama). Mfano wa viongozi hawa wa jadi nchini
              ni Mtemi Mirambo na Isike wa kabila la Wanyamwezi, Mutwa
              Mkwawa wa kabila la Wahehe, Omukama Rumanyika wa kabila

              la Wahaya, Mangi Meli wa Old Moshi, Mangi Sina wa Kibosho,
              Mangi Mareale wa Marangu na kadhalika.  Mamlaka za jadi
              zilikuwa na majukumu ya kuongoza shughuli zote za kisiasa,
              kiuchumi na kijamii pamoja na maadili katika jamii zao. Pia,

              zilikuwa na mamlaka juu ya rasilimali za jamii kama vile ardhi na
              mifugo. Vilevile, walimiliki miungu ya jamii. Kimsingi, mamlaka
              za jadi zilikuwa na nguvu. Hivyo, kuogopwa na watu wote katika
              jamii.


              Aidha,  mamlaka  hizo  zilishirikiana  na  baraza  lililoshirikisha
              viongozi wa koo zote katika kukuza na kutunza maadili ya jamii
              zao. Pia, zilishirikisha watu wenye maarifa mbalimbali katika

              kabila, kama vile waganga, watu wenye stadi na maarifa ya
              kiufundi, viongozi wa dini za jadi na watabiri katika ukuzaji na
              utunzaji wa maadili. Watabiri walitumika kutoa taarifa za mambo

              yajayo. Watu hawa walimsaidia kiongozi kwa karibu katika
              kutimiza majukumu yake.



                                                   138




                                                                                          06/11/2024   11:30:22
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   138
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   138                                    06/11/2024   11:30:22
   140   141   142   143   144   145   146   147   148   149   150