Page 149 - Historiayatznamaadili
P. 149

jamii nzima kufuata mila na desturi za jamii. Elimu ilisaidia
                    kurithisha maadili ya jamii kutoka kizazi kimoja hadi kingine.
                    Vijana walitegemewa na ukoo, kuendeleza mila, kanuni,
                    desturi na tunu walizorithishwa.
          FOR ONLINE READING ONLY
              (e)  Sanaa, ubunifu na michezo. Jamii za jadi hazikuwa na
                    mifumo ya kuandika na kusoma ili kutunza kumbukumbu
                    za maadishi kama ilivyo sasa. Hivyo, sanaa, ubunifu na
                    michezo vilitumika katika kukuza na kusimamia maadili.

                    Mifumo hii ilisimamiwa na mamlaka za jadi ili kuhakikisha
                    ushiriki wa jamii na utoaji wa taarifa zinazoendana na
                    maadili ya jamii husika. Pia, nyimbo zilitumika kuwasifu
                    watu wenye maadili au kuwakanya wasio na maadili.


                                Kazi ya kufanya namba 4

                           Jadili umuhimu wa kuendeleza mbinu zilizotumiwa

                           na mamlaka za jadi katika kukuza na kutunza maadili
                           kwa sasa.



              Sanaa, ubunifu na michezo katika kukuza na kutunza maadili

              Mfano wa mifumo ya sanaa, ubunifu na michezo iliyotumika ni

              kama ifuatavyo:

                  (i)  Uchoraji. Jamii zilichora michoro mbalimbali ili kuonesha
                        shughuli za jamii na maadili yake.  Michoro hii ilitumika
                        kama njia ya kutunza kumbukumbu kutoka kizazi kimoja
                        hadi kingine. Mfano wa michoro hii ni ile iliyopo mapango

                        ya Kondoa Irangi, Igeleke, Iringa, na Kombangulu, Kilolo.
                        Michoro hii ilitunzwa na kusimamiwa na mamlaka za jadi.
                        Kielelezo namba 1, kinaonesha michoro inayoelezea
                        shughuli za uchumi na maadili ya jamii.









                                                   142




                                                                                          06/11/2024   11:30:23
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   142                                    06/11/2024   11:30:23
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   142
   144   145   146   147   148   149   150   151   152   153   154