Page 151 - Historiayatznamaadili
P. 151

(iii)  Uchongaji.  Uchongaji  wa  vitu  kama  vile  vinyago
                        ulifanyika ili kuonesha maisha mbalimbali ya jamii. Kuna
                        vinyago vilivyochongwa ili kusisitiza umoja, ushirikiano
                        au upole. Vingine vilionesha heshima, utii kwa wakubwa,
          FOR ONLINE READING ONLY
                        kusaidia wasiojiweza na kupendana. Mbinu hii ilisaidia
                        kutoa taarifa na kutunza kumbukumbu za jamii kwani
                        vinyago vilidumu hadi vizazi vilivyofuata, hasa vile
                        vilivyochongwa kwenye mti mgumu au jiwe. Kielelezo

                        namba 2, kinaonesha vinyago vyenye kutoa ujumbe
                        wa maadili ya jamii.

























              Kielelezo namba 2: Vinyago vyenye ujumbe wa mila na desturi za jamii

                      Zoezi namba 3

                1.  Orodhesha vitu unavyoviona katika picha namba 1, 2

                      na 3.
                2.  Eleza tafsiri ya vitu ulivyoorodhesha katika swali la 1.



                  (iv)  Simulizi. Simulizi mbalimbali kama vile, riwaya (hadithi),
                        tamthiliya, michezo ya kuigiza, ushairi, na ngano zenye
                        maudhui mahususi ya maadili kwa jamii zilitumika
                        kukuza na kutunza maadili ya jamii husika. Simulizi
                        hizi ziliwafundisha watu maadili ya jamii. Kadiri simulizi
                        zilivyosimuliwa, zilirithishwa kizazi kimoja hadi kingine.



                                                   144




                                                                                          06/11/2024   11:30:24
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   144                                    06/11/2024   11:30:24
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   144
   146   147   148   149   150   151   152   153   154   155   156