Page 154 - Historiayatznamaadili
P. 154

adhabu kwa usawa kulingana na kosa husika. Mamlaka
                    za jadi zilikuza na kusimamia maadili ya jamii kwa maslahi
                    ya jamii zao. Misingi hii ilisaidia kuwapo kwa uaminifu na
                    heshima pale viongozi wa jamii waliposisitiza na kusimamia
          FOR ONLINE READING ONLY
                    ukuzaji na utunzaji wa maadili ya jamii.

              (c)  Umoja. Viongozi wa jadi walisimamia maadili kwa kushirikina
                    na mamlaka zingine kuanzia ngazi ya familia na ukoo. Hii
                    ilirahisisha ukuzaji na utunzaji wa maadili katika jamii nzima.
                    Baadhi ya makosa yalipotokea, familia au ukoo uliwajibika
                    kwa kutokukuza na kutunza maadili katika ngazi zao. Hii
                    ilisababisha mamlaka za familia na koo kuwa mstari wa
                    mbele katika kusimamia ukuzaji na utunzaji wa maadili

                    katika jamii.

                                Kazi ya kufanya namba 8

                           Jadili mambo uliyojifunza kuhusu misingi ya ukuzaji

                           na utunzaji wa maadili iliyotumiwa na mamlaka za
                           jadi na jinsi ya kuiendeleza kwa sasa.



              Wajibu wa mtoto katika kukuza na kutunza maadili

                                Kazi ya kufanya namba 9

                           Fikiri  na  andika wajibu wako katika kukuza na

                           kutunza maadili ya jamii kwa sasa.




              Ukuzaji na utunzaji wa maadili katika jamii ni jukumu la kila mtu.
              Hivyo, kama mtoto unao wajibu wa kufanya mambo yafuatayo
              katika kukuza na kutunza maadili ya jamii:

              (a)  Kujifunza.  Mtoto anaweza kujifunza maadili akiwa
                    nyumbani, shuleni na katika jamii inayomzunguka. Mtoto
                    anaweza kujifunza maadili ya jamii kwa kusikiliza, kusoma

                    ama kuiga vitendo vya kimaadili kutoka kwa wazazi, walezi,



                                                   147




                                                                                          06/11/2024   11:30:24
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   147                                    06/11/2024   11:30:24
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   147
   149   150   151   152   153   154   155   156   157   158   159