Page 153 - Historiayatznamaadili
P. 153

Kazi ya kufanya namba 7

                           Fanya uchunguzi kuhusu maana ya ngoma

                           zinazochezwa katika jamii yako ukizingatia midundo
                           na maneno ya nyimbo hizo na nafasi yake katika
          FOR ONLINE READING ONLY
                           kukuza na kutunza maadili.


              Misingi ya mamlaka za jadi katika ukuzaji na utunzaji wa
              maadili

              Mamlaka za jadi zilisimamia misingi mbalimbali katika ukuzaji
              na utunzaji wa maadili. Misingi hiyo ni kama ifuatavyo:

              (a)  Heshima. Utunzaji na ukuzaji wa maadili ulisimamiwa
                    katika misingi ya heshima. Mamlaka za jadi na jamii

                    nzima ziliheshimu misingi ya maadili iliyokuwapo katika
                    jamii. Mamlaka za jadi zilifuata sheria, mila na desturi
                    walizorithishwa na mababu na mabibi zao. Mamlaka za

                    jadi zilisimamia na kuhakikisha kila mwanajamii anazifuata.
                    Pale, ilipotokea ukiukwaji wa maadili, viongozi walichukua
                    hatua za kinidhamu dhidi ya wahusika ili kukuza na kutunza
                    maadili ya jamii zao.


                      Zoezi namba 4

                1.  Eleza  umuhimu  wa  viongozi  kuendelea  kuheshimu

                      maadili ya jamii katika ukuzaji na utunzaji wa maadili ya
                      jamii kwa sasa.
                2.  Eleza hasara za kutokuhesimu maadili ya jamii katika
                      kukuza na kutunza maadili.



              (b)  Uadilifu. Uadilifu uliheshimiwa katika ukuzaji na utunzaji
                    wa maadili. Usimamizi wa maadili ulifanyika katika misingi

                    ya uwazi, ukweli na haki kwa watu wote. Hapakuwa na
                    upendeleo katika utoaji wa adhabu na kukemea vitendo
                    vilivyokuwa kinyume na maadili. Kila mtu alipewa onyo na



                                                   146




                                                                                          06/11/2024   11:30:24
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   146
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   146                                    06/11/2024   11:30:24
   148   149   150   151   152   153   154   155   156   157   158