Page 155 - Historiayatznamaadili
P. 155

walimu, na watu wengine katika jamii inayomzunguka.
                    Hivyo, mtoto anapaswa kuwa msikivu ili kujifunza maadili
                    ya jamii yake na kutoka kwa viongozi waliopo;

              (b)  Kutii sheria, kanuni na taratibu za jamii yake. Utii wa
          FOR ONLINE READING ONLY
                    sheria na kanuni utamwezesha mtoto kuishi kulingana na
                    mila na desturi za familia, ukoo, jamii na Taifa kwa ujumla.
                    Pia, utamwezesha mtoto kuishi kwa amani katika jamii
                    inayomzunguka;


              (c)  Kulinda na kudumisha maadili ya jamii yake. Mtoto
                    anaweza kulinda maadili ya jamii kwa kuacha vitendo
                    vilivyo kinyume na maadili. Pia, mtoto anapaswa kukemea
                    vitendo vilivyo kinyume na maadili vinavyotendwa na watoto

                    wenzake na wanajamii. Mtoto anaweza kukemea kwa
                    kupinga na kukataa kushiriki vitendo hivyo;

              (d)  Kuripoti vitendo vilivyo kinyume na maadili. Mtoto anao
                    wajibu wa kutoa taarifa zinazohusu ukiukwaji wa maadili.

                    Mfano, anaweza kutoa taarifa kwa wazazi, walezi, walimu
                    na serikali za Mtaa/Kijiji. Pia, anaweza kutoa taarifa katika
                    mamlaka za kisheria kama vile, polisi, Taasisi ya Kuzuia

                    na Kupambana na Rushwa na Mamlaka ya Kudhibiti na
                    Kupambana na Dawa za Kulevya. Mtoto hapaswi kukaa
                    kimya au kuficha anapofanyiwa vitendo viovu na anapoona
                    vinafanyika; na


              (e)  Kuelimisha. Mtoto anaweza kuwaelimisha watoto wenzake
                    na jamii kwa ujumla kuhusu umuhimu wa kukuza na kutunza
                    maadili.

                                Kazi ya kufanya namba 10

                           Jadili na kuandika mikakati ya kutoa elimu ya kukuza

                           na kutunza maadili katika jamii.






                                                   148




                                                                                          06/11/2024   11:30:24
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   148                                    06/11/2024   11:30:24
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   148
   150   151   152   153   154   155   156   157   158   159   160