Page 150 - Historiayatznamaadili
P. 150

FOR ONLINE READING ONLY




















                             Kielelezo namba 1: Michoro ya mapangoni
                  (ii)  Muziki na nyimbo. Nyimbo zenye maudhui ya kukuza

                        na kutunza maadili ziliimbwa na kuchezwa katika
                        matukio ya kijamii. Kwa mfano, nyimbo zilizoimbwa
                        wakati wa harusi, zilieleza wanandoa namna ya kuishi

                        katika ndoa. Nyimbo zilizoimbwa wakati wa kulima na
                        mavuno zilieleza maadili katika kilimo. Vivyo hivyo,
                        nyimbo zilizoimbwa wakati wa kuzaliwa mtoto zililenga
                        malezi ya mtoto. Kila tukio lilikuwa na nyimbo zake na
                        zenye mafundisho ya kimaadili. Watu waliokiuka maadili

                        walitungiwa nyimbo za kuonya. Hii ilisababisha watu
                        kuzingatia maadili.


                                Kazi ya kufanya namba 5

                           Jadili nafasi chanya na hasi za muziki wa kizazi kipya
                           katika kukuza na kutunza maadili ya jamii nchini kwa
                           sasa.









                                                   143




                                                                                          06/11/2024   11:30:23
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   143                                    06/11/2024   11:30:23
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   143
   145   146   147   148   149   150   151   152   153   154   155