Page 148 - Historiayatznamaadili
P. 148

(b)  Kuonya kwa kukemea uvunjaji wa maadili ya jamii.
                    Yeyote aliyekiuka maadili ya jamii alipewa adhabu kali.
                    Baadhi ya adhabu zilitolewa mbele ya jamii nzima. Hii
                    ilisaidia watu kutambua athari za ukiukaji wa maadili katika
                    jamii.
          FOR ONLINE READING ONLY
              (c)  Vitisho. Vitisho vilikuwa njia mojawapo katika kukuza na
                    kutunza maadili. Vitisho vilitolewa vikiambatana na miiko
                    yenye mila na desturi ili kuifanya jamii kuogopa madhara
                    ya ukiukaji wa maadili. Miiko iliwekwa na ilisimamiwa na

                    mamlaka za jadi ili kukuza na kutunza maadili.


                      Zoezi namba 2


                1.  Andika miiko mitatu (3) iliyotumika kukuza na kutuza
                      maadili.

                2.  Fafanua maana ya miiko ifuatayo:

                       (i)  Usisimulie hadithi mchana utaota mkia.
                       (ii)  Usishone nguo ukiwa umevaa, utakuwa maskini.

                       (iii)  Usipige mluzi usiku, utamwita shetani.

                       (iv)  Usifagie usiku, utafukuza bahati.
                       (v)  Usimpige mwenzio kwa ufagio.

                3.  Eleza umuhimu wa matumizi ya miiko katika kukuza na
                      kutunza maadili.



              (d)  Elimu. Elimu ilitumika kama njia ya kukuza na kutunza
                    maadili. Watoto wadogo walifundishwa maadili na watu

                    wazima, ikiwemo wazazi wao. Pia, elimu za unyago na
                    jando zilitumika kukuza na kutunza maadili ya jamii. Pamoja
                    na kuwapo watu rasmi wa kutoa elimu za jando na unyago,

                    mamlaka za jadi zilisimamia ili kuhakikisha utekelezaji
                    wake katika jamii nzima. Elimu hii ilikuwa ya lazima kwa
                    kila mwanajamii. Maarifa na stadi zilizotolewa zilisaidia



                                                   141




                                                                                          06/11/2024   11:30:23
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   141                                    06/11/2024   11:30:23
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   141
   143   144   145   146   147   148   149   150   151   152   153