Page 146 - Historiayatznamaadili
P. 146

Mamlaka za jadi katika ukuzaji na utunzaji maadili

                                Kazi ya kufanya namba 3

                           Fanya uchunguzi kuhusu namna mamlaka za jadi
          FOR ONLINE READING ONLY
                           zilivyosimamia ukuzaji na utunzaji wa maadili katika
                           jamii yako.



              Mamlaka za jadi zilikuwa na mchango mkubwa katika ukuzaji
              na utunzaji wa maadili. Mamlaka za jadi zilisimamia ukuzaji na
              utunzaji wa maadili katika jamii. Aidha, mamlaka hizo zilikuwa
              ndiyo ngazi ya mwisho ya usimamizi wa maadili katika jamii.
              Mamlaka za jadi zilikuwa na majukumu yafuatayo katika kukuza

              na kutunza maadili yao.

              (a)  Kutunga sheria, kanuni na taratibu za jamii. Mamlaka
                    za jadi zilisimamia utungaji wa sheria, kanuni na taratibu
                    za jamii. Hii ilisaidia jamii zao kuwa na sheria, kanuni na
                    taratibu zilizotambuliwa na jamii nzima. Hivyo, ilikuwa
                    wajibu kisheria kwa jamii nzima kuzingatia mila na desturi
                    zilizokubalika katika jamii. Aidha, mamlaka hizi zilikuwa
                    na wajibu wa kubadilisha sheria au kanuni zisizofaa au
                    ambazo zimepitwa na wakati, hazina tija, haziendani na

                    mazingira au hazikukidhi matakwa ya jamii zao. Hii ilisaidia
                    kukuza maadili yaliyoendana na wakati katika jamii zao.

              (b)  Kusimamia maadili ya jamii. Mamlaka za jadi ndizo
                    zilizosimamia ukuzaji na utunzaji wa maadili. Jambo la
                    kimaadili liliposhindikana katika ngazi za chini, lilipelekwa
                    katika mamlaka hizo kwa utatuzi. Mamlaka za jadi zilikuwa
                    na maamuzi ya juu.

              (c)  Kusimamia shughuli za kimila, kama vile ibada,
                    matambiko na dini za jadi. Hii ni kutokana na ukweli kuwa
                    mamlaka hizi zilikuwa na watu wenye nguvu za miungu ya
                    kabila.  Hii ilisaidia jamii nzima kuthamini mila na desturi
                    zao na kuzifuata.




                                                   139




                                                                                          06/11/2024   11:30:23
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   139
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   139                                    06/11/2024   11:30:23
   141   142   143   144   145   146   147   148   149   150   151