Page 160 - Historiayatznamaadili
P. 160

Kazi ya kufanya namba 2

                           Fanya uchunguzi wa Nembo ya Taifa, kisha andika

                           vitu vilivyopo katika nembo hiyo.
          FOR ONLINE READING ONLY

              Nembo ya Taifa ina alama mbalimbali kama vile bibi na bwana,

              mwenge, bendera ya Taifa, jembe na nyundo, milia ya bluu,
              pembe  za  ndovu,  mlima, mkuki,  karafuu, pamba, rangi  ya
              dhahabu (njano) na maneno “uhuru na umoja”.


                                Kazi ya kufanya namba 3

                           Jadili na andika maana ya alama zilizopo katika
                           nembo ya Taifa.



              Alama zilizopo katika nembo ya Taifa zina maana mahususi

              katika utambulisho wa historia ya Taifa la Tanzania. Alama hizi
              zina utambulisho wa watu, historia ya nchi na rasilimali zilizopo
              nchini.  Mfano, alama ya Bendera ya Taifa inaashiria uhuru wa

              Taifa letu. Alama ya watu wawili; mtu mume na mke ambao
              wameshika ngao ni ishara ya kusisitiza usawa na ushirikiano
              wa jinsi zote katika jamii yetu ya Kitanzania. Alama ya mlima,
              ni ishara ya uwepo wa mlima mrefu wa Kilimanjaro, ambao ni
              fahari kwa nchi ya Tanzania.  Mlima Kilimanjaro ni mlima mrefu

              kuliko yote barani Afrika. Pamba na karafuu huwakilisha mazao
              muhimu ya biashara yanayopatikana katika nchi yetu.  Alama
              ya mwenge ni kiashirio cha ishara ya uhuru wetu. Mwenge huu

              uliwashwa kwa mara ya kwanza juu ya mlima Kilimanjaro wakati
              nchi ilipopata uhuru.

              Rangi ya njano (dhahabu) ni alama inayoashiria uwepo wa

              rasilimali za madini ya dhahabu nchini.  Alama ya jembe na
              shoka husisitiza umuhimu wa kazi kama msingi wa ujenzi wa
              maisha ya Mtanzania.  Alama ya mkuki na ngao vinawakilisha



                                                   153




     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   153                                    06/11/2024   11:30:25
                                                                                          06/11/2024   11:30:25
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   153
   155   156   157   158   159   160   161   162   163   164   165