Page 164 - Historiayatznamaadili
P. 164

Kazi ya kufanya namba 6

                           Chunguza, kisha andika shughuli zinazoambatana
                           na tukio  la  mwenge  wa  uhuru  katika  eneo

                           linalokuzunguka.
          FOR ONLINE READING ONLY

              Mnyama twiga

              Mnyama Twiga ni alama ya utambulisho wa Taifa. Alama hii
              ni kiashirio cha uwepo wa mbuga zenye wanyama mbalimbali
              nchini Tanzania. Twiga ni mnyama anayeashiria amani licha ya

              ukubwa wake. Tanzania ina mbuga za wanyama zenye wanyama
              wa aina tofauti. Kielelezo namba 5, kinaonesha picha ya Twiga.

              Mbuga za wanyama ni fahari ya nchi yetu. Tanzania ina mbuga

                                                     za wanyama kama vile,
                                                     Ngorongoro, Manyara, Mikumi,
                                                     Tarangire,  Ruaha,  Serengeti,
                                                     Jozani        (Unguja),        Ngezi
                                                     (Pemba), Rubondo na Saanane.

                                                     Licha ya mbuga  hizi kuna
                                                     mapori tengefu mengi. Mfano,
                                                     takribani asilimia 28 ya maeneo

                                                     ya ardhi nchini yamehifadhiwa
                                                     kwa ajili ya mbuga na hifadhi za
                   Kielelezo namba 5:
                      Mnyama Twiga                   wanyamapori.

                                Kazi ya kufanya namba 7


                           Andika  orodha  ya  wanyamapori  wanaopatikana
                           nchini Tanzania.



              Watalii wengi huja kutembelea mbuga hizi kwa ajili ya kuona
              wanyama. Watalii hawa hulipatia Taifa fedha za kigeni. Hivyo,
              kuinua pato la Taifa.



                                                   157




                                                                                          06/11/2024   11:30:26
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   157
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   157                                    06/11/2024   11:30:26
   159   160   161   162   163   164   165   166   167   168   169