Page 166 - Historiayatznamaadili
P. 166

Kazi ya kufanya namba 8

                           Chunguza noti ya shilingi 10,000, 5,000 na 2,000
                           na sarafu ya shilingi 500, 200 na 100 kisha andika
                           alama zilizopo.
          FOR ONLINE READING ONLY

              Fedha za Tanzania zina alama zenye viongozi wakuu wa nchi
              na rasilimali zilizopo nchini. Fedha zinapaswa kuheshimiwa

              katika matumizi na kwa ajili ya ustawi wa mtu binafsi, jamii na
              Taifa kwa ujumla. Fedha hutumika kwa ajili ya kupata huduma
              kama vile chakula, malazi, mavazi, elimu na mahitaji mengine
              ya jamii.  Hivyo, ni kosa la jinai kwa mtu yeyote kutokuheshimu

              fedha hizi, kutupa, kuchana au kuchafua fedha kwa makusudi.

              Sikukuu za Kitaifa
              Sikukuu za Kitaifa ni alama muhimu zilizobeba utambulisho

              wa Taifa la Tanzania. Sikukuu hizi ni zile zenye matukio yenye
              kuonesha kumbukumbu za kihistoria nchini.

                                Kazi ya kufanya namba 9


                           Jadili  na  andika  sikukuu  za  Kitaifa  nchini  na
                           kumbukumbu zilizoambana nazo.


              Sikukuu za Kitaifa hutambulika nchini na huadhimishwa kila

              mwaka. Orodha ifuatayo inaonesha sikukuu za kitaifa nchini:
                  (a)  9 Disemba. Hii ni sikukuu ya kitaifa, yenye kumbukizi

                       ya kihistoria, ambapo nchi ya Tanganyika ilipata uhuru;

                  (b)  12 Januari, ni sikukuu ya kitaifa, yenye kumbukizi ya
                       kihistoria, ya siku ya Mapinduzi ya Zanzibar yalipofanyika.
                       Mapinduzi haya yalifanyika ili kuondoa utawala wa
                       kisultani na kuweka utawala wa Wazanzibari. Mapinduzi

                       haya yalikuwa ni muhimu katika kupata uhuru rasmi.
                       Wazanzibari hawakuwa na uhuru kamili, kwa sababu nchi
                       hii ilipopewa uhuru, madaraka yalibaki kwa sultani; na


                                                   159




     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   159                                    06/11/2024   11:30:26
                                                                                          06/11/2024   11:30:26
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   159
   161   162   163   164   165   166   167   168   169   170