Page 161 - Historiayatznamaadili
P. 161

silaha za jadi za ulinzi kama nyenzo za ulinzi nchini. Milia ya
              bluu inawakilisha rasilimali za maji kama vile bahari, mito na
              maziwa nchini. Alama ya pembe za ndovu inaonesha uwapo wa
              utajiri mkubwa wa wanyama katika nchi ya Tanzania. Maneno
          FOR ONLINE READING ONLY
              “UHURU NA UMOJA” ni alama inayosisitiza uhuru na umoja wa
              watu wa Tanzania.

              Nembo ya Taifa ina alama zenye utambulisho wa rasilimali za

              Taifa, matukio ya Kihistoria, utajiri wa Taifa letu na maadili ya
              Taifa. Kimsingi, Nembo ya Taifa hutoa utambulisho wa Taifa
              ndani na nje ya mipaka ya nchi.


              Bendera ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

              Bendera ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ina alama zenye
              utambulisho wa Taifa.

                                Kazi ya kufanya namba 4

                           Chunguza bendera ya Taifa, kisha andika maana ya
                           rangi zilizopo katika bendera hiyo.




              Bendera ya Taifa ni alama ya utambulisho wa Jamhuri ya
              Muungano wa Tanzania kama Taifa huru. Kielelezo namba 2,
              kinaonesha Bendera ya Taifa.

                                                   Bendera ina rangi nne ambazo
                                                   zinatambulisha Taifa letu. Rangi
                                                   nyeusi inawakilisha alama ya
                                                   uwepo  wa watu  wenye asili
                                                   ya Kiafrika. Rangi ya kijani

                                                   inawakilisha ardhi na uoto wa
                                                   asili. Rangi ya bluu (samawati)
                                                   inawakilisha utajiri wa maji:
                                                   bahari, maziwa na mito iliyopo
                      Kielelezo namba 2:           ndani ya nchi na inayolizunguka
                       Bendera ya Taifa            Taifa la Tanzania.



                                                   154




                                                                                          06/11/2024   11:30:25
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   154                                    06/11/2024   11:30:25
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   154
   156   157   158   159   160   161   162   163   164   165   166