Page 167 - Historiayatznamaadili
P. 167

(c)  26 Aprili, ni sikukuu ya kitaifa yenye kumbukizi ya
                       kihistoria ambapo Tanganyika na Zanzibar ziliungana
                       na kuzaliwa kwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa
                       Tanzania.
          FOR ONLINE READING ONLY
              Sikukuu hizi ndizo muhimu kwa historia ya Mtanzania katika
              kupata uhuru na kuwa Taifa huru. Pia, zipo sikukuu zingine za
              kitaifa kama siku za wafanyakazi (Mei mosi), wafanyabiashara
              (Sabasaba) na wakulima (Nanenane).


              Matumizi ya alama za Taifa

              Alama za Taifa ni muhimu katika utambulisho wa Taifa la
              Tanzania. Hivyo, alama hizo hutumika katika shughuli za kitaifa
              na nyaraka za kitaifa.


                                Kazi ya kufanya namba 10


                           Jadili matumizi ya alama za Taifa.






              Alama za Taifa hutumika katika maeneo kadhaa kutambulisha
              nchi ya Tanzania. Kwa mfano, nembo ya Taifa, huwekwa katika
              nyaraka muhimu za nchi ili kuzitambulisha kuwa ni mali ya Taifa

              na siyo mali ya mtu binafsi. Nembo hii hutumika pia katika
              barua za kiserikali ili kuitambulisha serikali. Nembo hii huashiria
              umuhimu wa nyaraka husika kwa Taifa.


              Pia, bendera ya Tanzania hutumika katika ofisi za serikali,

              mikutano na ziara za kiserikali ili kulitambulisha Taifa la Tanzania.
              Kila watu waonapo bendera hii hutambua uwapo wa Taifa la
              Tanzania. Aidha, fedha za Tanzania, hutumika kama alama ya

              kuhalalisha matumizi ya fedha husika katika shughuli mbalimbali.






                                                   160




     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   160                                    06/11/2024   11:30:26
                                                                                          06/11/2024   11:30:26
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   160
   162   163   164   165   166   167   168   169   170