Page 103 - Historiayatznamaadili
P. 103

Zoezi namba 6


                1.  Ainisha maadili yaliyozingatiwa katika shughuli za uchumi
                      ili kutunza afya ya jamii.
          FOR ONLINE READING ONLY
                2.  Fafanua umuhimu wa maadili katika shughuli za uchumi
                      katika kutunza afya ya jamii.


              Matumizi ya mifumo ya imani za jadi

              Maadili katika shughuli za uchumi yalitumia mifumo ya imani za
              jadi. Mfano, ibada zilizohusisha matambiko maalumu zilifanyika
              kabla ya kuanza shughuli za uchumi. Ibada zilifanyika kwa lengo
              la kuomba baraka katika utendekaji wa kazi na kuomba mavuno
              mengi. Pia, ibada zilifanyika kuondoa vikwazo katika shughuli

              za uchumi. Mfano, jamii za wahunzi zilifanya ibada ili kutakasa
              rasilimali watu na vifaa katika shughuli za uhunzi. Vilevile, ibada
              zilifanyika baada ya shughuli za uchumi ili kuishukuru miungu
              kwa kupata mavuno mengi. Baadhi ya jamii, zilitoa mavuno ya
              kwanza kama sadaka ya miungu wao.


              Maadili katika kazi

              Maadili katika shughuli za uchumi yalizingatia jinsi. Palikuwapo
              na kazi zilizofanywa na wanawake na zile za wanaume. Mipaka
              iliwekwa katika jinsi kwa ajili ya ustawi wa jamii na usalama.

              Wanawake hawakuhusishwa katika baadhi ya shughuli kwa
              ajili ya ulezi wa watoto na familia. Baadhi ya shughuli kama vile
              uhunzi, uwindaji na ufugaji zilihitaji kutembea na kukaa porini

              muda fulani. Hali hii ilionekana kuwa ngumu kwa wanawake
              kwa sababu ya ulezi wa familia na watoto.

              Maadili katika jamii pia yalisisitiza kila mwanajamii kufanya kazi

              ili kuendeleza shughuli za uchumi katika jamii zao. Watu ambao
              hawakufanya kazi walikuwa ni wazee, watoto na wagonjwa.
              Jamii zilithamini kazi; kazi ilikuwa kipimo cha utu. Pia, jamii
              zilifanya shughuli za uchumi kwa kushirikiana ambapo wanajamii



                                                   96




                                                                                          06/11/2024   11:30:15
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   96
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   96                                     06/11/2024   11:30:15
   98   99   100   101   102   103   104   105   106   107   108