Page 100 - Historiayatznamaadili
P. 100

Hii ilisababisha shughuli za uchumi kukua ili kukidhi mahitaji ya
              jamii.

              Shughuli za uchumi zilisaidia kukua kwa shughuli zingine
              za uchumi. Mfano,viwanda vya zana za chuma viliwezesha
          FOR ONLINE READING ONLY
              wakulima kulima eneo kubwa zaidi. Hivyo, kupata chakula cha
              kutosha kulisha jamii zao na kuwa na ziada. Pia, viwanda hivi
              vilisaidia kukua kwa shughuli za uvuvi, uchongaji na uwindaji.

              Vilevile,viwanda vya ususi, chumvi na uchongaji vilisaidia kukua
              kwa shughuli za uvuvi. Aidha, shughuli za uchumi zilichangia
              kukua kwa shughuli za biashara.Jamii zilibadilishana ziada ili
              kupata vitu vingine kutoka jamii zingine. Vivyo hivyo, wafugaji
              walibadilishana maziwa na mifugo kwa nafaka kutoka kwa
              wakulima. Wavuvi walibadilishana samaki ili kupata nafaka
              kutoka kwa wakulima. Hii iliimarisha biashara kati ya jamii na
              jamii. Shughuli za uchumi zilizisaidia jamii kukidhi mahitaji yao
              kabla ya kuja kwa ukoloni.


              Shughuli za uchumi zilisababisha jamii za kale kujenga makazi
              ya kudumu. Kuimarika kwa makazi kulisababisha kukua na
              kuimarika kwa mamlaka za jadi. Kwa ujumla, shughuli za uchumi
              zilichangia kukua kwa shughuli nyingine za uchumi, kuimarika
              kwa makazi ya jamii, kukua kwa mamlaka za jadi na kukuza
              uhusiano kati ya jamii. Hivyo kuleta maendeleo kabla ya kuja
              kwa wakoloni nchini.

              Maadili katika shughuli za uchumi

                                Kazi ya kufanya namba 11


                           Fanya  uchunguzi  kuhusu  shughuli  za  uchumi
                           zinazofanyika katika eneo linalokuzunguka, kisha
                           andika maadili yake.



              Maadili katika shughuli za uchumi yalilenga katika kulinda
              rasilimali asilia za uchumi, kuomba baraka za mavuno, kutunza
              afya ya jamii, kujenga ushirikiano na uhusiano katika kazi na
              uhifadhi wa maarifa na ujuzi wa jamii husika. Jamii zilitambua


                                                   93




                                                                                          06/11/2024   11:30:15
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   93
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   93                                     06/11/2024   11:30:15
   95   96   97   98   99   100   101   102   103   104   105