Page 98 - Historiayatznamaadili
P. 98

Bidhaa za uchongaji zilikuwa kwa ajili ya matumizi ya jamii na
              kwa ajili ya biashara ili kupata bidhaa ambazo hazikuwapo katika
              jamii zao.

                                Kazi ya kufanya namba 8
          FOR ONLINE READING ONLY

                           Fanya uchunguzi kwa kuuliza, kusoma matini au
                           kutembelea maeneo yenye shughuli za uchumi za
                           uchongaji, kisha eleza namna jamii inavyoziendeleza

                           kwa sasa.



              Shughuli za uchumi katika uchongaji zilikuwapo kabla ya ujio
              wa wakoloni nchini. Shughuli za uchumi katika uchongaji bado
              zinaendelea katika jamii zetu mpaka sasa. Watalii hupendelea
              kununua vitu vya kuchongwa kwa ajili ya mapambo na matumizi

              mengine ya nyumbani hadi sasa.

              Mzee Kukawa alihitimisha simulizi na wageni wote walishangilia
              kwa nderemo na vifijo.

                                Kazi ya kufanya namba 9


                           Andika jinsi ya kuendeleza shughuli za uchumi katika
                           uchongaji kwa maendeleo ya uchumi na jamii kwa
                           sasa.



              Shughuli za uchumi za utengenezaji wa chumvi

              Mzee aliyefuata alikuwa Mzee Kware kutoka maeneo ya Uvinza,
              mkoa wa Kigoma. Mzee huyu aliwakilisha shughuli za uchumi za
              utengenezaji chumvi. Mzee Kware alianza kwa kuelezea kuwa:

              Shughuli za utengenezaji chumvi zilikuwa shughuli kuu ya uchumi
              kwa jamii zilizoishi maeneo yenye maji yenye asili ya chumvi.

              Mfano, wa jamii hizo ni za Uvinza huko Kigoma zinazoishi kando
              ya mto Malagarasi. Jamii zingine ni zile zinazoishi Ivuna, Rukwa,
              Ziwa Eyasi, Ziwa Balangida na Kitangiri.



                                                   91




                                                                                          06/11/2024   11:30:15
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   91
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   91                                     06/11/2024   11:30:15
   93   94   95   96   97   98   99   100   101   102   103