Page 99 - Historiayatznamaadili
P. 99

Shughuli za utengenezaji wa chumvi zilifanyika kwa ajili ya kukidhi
              mahitaji ya jamii na biashara. Mfano, chumvi iliyotengenezwa
              Uvinza ilikuwa bidhaa muhimu sana wakati wa biashara za jamii
              na zile za masafa marefu. Jamii hizo zilibadilishana chumvi na
              jamii zilizowazunguka na zile za mbali ili kupata bidhaa zingine.
          FOR ONLINE READING ONLY
              Wafanyabiashara kutoka maeneo mbalimbali walihitaji chumvi ili
              kubadilishana na chakula wakiwa njiani. Karibu kila jamii ilihitaji

              chumvi kama ilivyohitaji zana za chuma.

                                Kazi ya kufanya namba 10

                           Andika jinsi ya kuendeleza shughuli ya utengenezaji
                           chumvi kwa maendeleo ya uchumi na jamii kwa sasa.





              Mzee Kware alihitimisha huku watu wote wakimpigia makofi na
              vifijo.

                      Zoezi namba 4

                1.  Eleza mchango wa viwanda vya ususi katika maendeleo
                      ya uvuvi kabla ya ukoloni.

                2.  Fafanua namna viwanda vya uchongaji vilivyosaidia
                      maendeleo ya uvuvi kabla ya ukoloni.
                3.  Ni kwa namna gani matumizi ya moto na chumvi
                      yalivyosaidia kukua kwa uvuvi nchini kabla ya ukoloni?



              Mchango wa shughuli za uchumi katika maendeleo ya jamii

              Shughuli za uchumi zilikuwa na mchango mkubwa katika
              maendeleo  ya  jamii  kabla  ya  ukoloni.  Shughuli  za  uchumi
              katika jamii zilitegemeana ili kukidhi mahitaji yake. Mfano, jamii
              zilizotengeneza chumvi zilitegemea wakulima ili kupata chakula.
              Pia, wakulima walitegemea jamii za wahunzi ili kupata majembe,

              mashoka, mapanga na zana nyinginezo kwa ajili ya shughuli za
              kilimo. Aidha, viwanda vya uchongaji vilitegemea viwanda vya
              uhunzi na viwanda vya ususi vilitegemea wakulima na kadhalika.



                                                   92




                                                                                          06/11/2024   11:30:15
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   92
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   92                                     06/11/2024   11:30:15
   94   95   96   97   98   99   100   101   102   103   104