Page 91 - Historiayatznamaadili
P. 91

Shughuli za uvuvi zilifanywa na jamii za watu walioishi maeneo ya
              Pwani ya Bahari ya Hindi. Pia, zilifanyika katika maeneo ya bara
              yenye maziwa makubwa kama vile ziwa Victoria, Tanganyika,
              na Nyasa.  Vilevile, uvuvi ulifanyika katika mito mikubwa kama
          FOR ONLINE READING ONLY
              vile mto Rufiji, Ruvuma, Malagarasi na Pangani. Jamii zilizoishi
              maeneo ya mwambao wa bahari na ziwa ndizo zilizovua samaki
              kwa wingi zaidi.


                                     Kazi ya kufanya namba 3

                            Chunguza ramani ya Tanzania, kisha onesha
                            maeneo yenye bahari, mito na maziwa yaliyohusika
                            na shughuli za uvuvi.



              Shughuli za uchumi za uvuvi zilifanyika kwa kutumia nyavu za asili
              na mitego mbalimbali. Nyavu zilizotumika zilitengenezwa kwa
              kutumia nyuzi za asili kama vile kamba za mimea na magamba
              ya miti. Pia, zilitumia mitego iliyotengenezwa kwa kutumia mianzi

              na fito. Wavuvi wengine walitumia mimea iliyokuwa na dawa ya
              kulevya samaki, kisha kuwavua. Vilevile, ndoano zilitumika katika
              shughuli za uvuvi. Nyavu na mitego vilitumika kunasa samaki
              wakubwa na wadogo. Mitumbwi na ngalawa iliyojengwa kwa miti
              ilitumika katika shughuli za uvuvi. Vyombo hivi vilitumika kwa
              ajili ya kusafiria kwenye maji yenye kina kirefu ili kuvua samaki
              wengi na wakubwa zaidi. Pia, dau za asili zilitumika kwa ajili ya

              shughuli za uvuvi na usafiri katika bahari na mito mikubwa.

              Ugunduzi wa chumvi na moto pia ulisaidia zaidi katika maendeleo
              ya shughuli za uvuvi. Chumvi na moto vilitumika kuhifadhia
              samaki kwa matumizi ya baadaye. Kwa ujumla, matumizi ya
              vifaa na zana katika shughuli za uvuvi na ugunduzi wa chumvi

              na moto vilisaidia maendeleo katika shughuli za uvuvi. Jamii za
              wavuvi zilivua samaki wengi na kuwa na ziada.

              Wavuvi walibadilishana ziada ya samaki na wakulima ili kupata
              nafaka. Pia, walibadilishana samaki ili kupata nyavu za kuvulia




                                                   84




                                                                                          06/11/2024   11:30:12
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   84
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   84                                     06/11/2024   11:30:12
   86   87   88   89   90   91   92   93   94   95   96