Page 63 - Historiayatznamaadili
P. 63

FOR ONLINE READING ONLY

















                     Kielelezo namba 10: Bwawa lililojengewa ukingo wa mawe

              Maji yaliyohifadhiwa katika bwawa yalitumika kwa umwagiliaji
              kipindi cha ukame. Watu hawakuruhusiwa kutumia maji haya
              wakati wa mvua. Hii ilisaidia jamii kupata mazao muda wote.
              Sayansi  na  teknolojia  hii  ilifanyika  maeneo  ya  Engaruka,

              Kaskazini mwa Tanzania katika jamii za Wairaqw. Pia, jamii ya
              Wasonjo ilitumia sayansi na teknolojia hii.


              Pia, baadhi ya jamii zilifanya umwagiliaji kwa kutumia mifereji
              asilia ya kuchimba. Mifereji hii ilitoka katika vyanzo vya maji,
              hasa katika maporomoko ya maji na milima na kutiririsha maji

              hadi maeneo ya mashamba. Jamii zilizotumia teknolojia hii ni
              Wapare na Wachaga.


              Kilimo asilia kwa kutumia matuta
              Maeneo yenye miinuko na mmomonyoko wa udongo, watu
              walilima kwa kutumia matuta ya kukingama. Jamii kama vile

              Wamatengo walitumia kilimo cha “ngoro”. Kilimo hiki kilifanyika
              katika maeneo yenye mteremko ili kuzuia mmonyoko wa udongo
              na kuiweka ardhi katika hali ya unyevunyevu. Kilimo cha ngoro
              kilifanyika kwa kutandika nyasi katikati kwa umbo la mstatili,




                                                   56




                                                                                          06/11/2024   11:29:54
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   56
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   56                                     06/11/2024   11:29:54
   58   59   60   61   62   63   64   65   66   67   68