Page 62 - Historiayatznamaadili
P. 62

ni utengenezaji wa zana za chuma. Kimsingi zana za chuma
              zilisaidia kurahisisha shughuli kama vile uvuvi, kilimo, uwindaji
              na shughuli nyingine za uzalishaji mali katika jamii.


                                Kazi ya kufanya namba 4
          FOR ONLINE READING ONLY
                           Jadili namna ya kuendeleza sayansi na teknolojia
                           ya ufuaji wa chuma kwa sasa.





              Sayansi na teknolojia asilia katika kilimo

              Kilimo ni mojawapo ya shughuli za kale iliyofanywa na jamii

              nyingi za Tanzania kabla ya ukoloni.

              Kilimo kwa kutumia zana asilia

              Sayansi na teknolojia katika kilimo awali ilifanyika kwa kutumia
              mawe na vijiti ili kuchimba na kufukua ardhi kwa lengo la kupanda
              mbegu. Mabaki ya majivu yalitumika kama mbolea. Sayansi na
              teknolojia hii ilikuwapo wakati wa Zama za Mawe za Mwisho;
              binadamu alipoanza kutumia zana za mawe kwa ajili ya kulimia.
              Aidha, sayansi na teknolojia za kilimo zilibadilika katika kipindi
              cha ugunduzi wa chuma, kutokana na kuanza kutumika kwa zana
              za chuma kama vile majembe, mapanga, mashoka na mundu
              katika kilimo.  Kipindi hicho, majembe yalitumika kuchimba na

              kufukua ardhi kwa ajili ya kilimo. Mapanga, mashoka na mundu
              vilitumika kufyeka majani, kukata miti ili kutayarisha shamba
              kwa ajili ya kilimo.


              Kilimo asilia cha umwagiliaji
              Vilevile, sayansi na teknolojia asilia ya umwagiliaji ilitumika katika

              shughuli za kilimo. Umwagiliaji ulifanyika kwa kuhifadhi maji
              kwenye mabwawa yaliyojengewa kingo kwa mawe wakati wa
              mvua za msimu. Kielelezo namba 10, kinaonesha mfano wa
              bwawa lililojengewa kingo za mawe kwa ajili ya kuhifadhi maji

              ya umwagiliaji.


                                                   55




                                                                                          06/11/2024   11:29:54
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   55
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   55                                     06/11/2024   11:29:54
   57   58   59   60   61   62   63   64   65   66   67