Page 58 - Historiayatznamaadili
P. 58

Sayansi na teknolojia asilia za Zama za Chuma

              Sayansi na teknolojia asilia za Zama za Chuma zilihusika katika
              kutengeneza zana mbalimbali za chuma. Chuma kilipatikana
              kwa kuchimba udongo (mbale) wenye chembechembe za madini
          FOR ONLINE READING ONLY
              ya chuma, kisha kuwekwa kwenye tanuru la moto mkali wa mkaa
              ili kuuyeyusha. Sayansi na teknolojia hii ilisababisha madini ya
              chuma yaliyochanganyikana na udongo kujitenga na kupata
              majimaji ya chuma yaliyoganda katikati ya tanuru, mfano wa

              mafukuto ya chuma safi yaliyoitwa kitali. Kitali kilitumika katika
              kutengeneza zana za chuma. Kielelezo namba 6, kinaonesha
              sayansi na teknolojia za ufuaji wa chuma.

































                     Kielelezo namba 6: Sayansi na teknolojia ya ufuaji chuma


              Kazi ya utengenezaji zana za chuma ilifanywa na wahunzi.
              Zana za chuma zilitengenezwa kwa kutumia nyundo na mawe ili

              kupata umbo husika. Moto ulitumika kuyeyusha chuma wakati wa
              utengenezaji wa zana. Kielelezo namba 7, kinaonesha shughuli
              za utengenezaji wa zana za chuma.




                                                   51




                                                                                          06/11/2024   11:29:53
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   51                                     06/11/2024   11:29:53
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   51
   53   54   55   56   57   58   59   60   61   62   63