Page 61 - Historiayatznamaadili
P. 61

Maadili katika sayansi na teknolojia asilia ya ufuaji wa chuma
              Sayansi na teknolojia ya asili katika utengenezaji wa zana za
              chuma ilihusisha maadili. Wahunzi walisali, walifanya matambiko,

              waliimba na kunywa dawa za asili kabla ya kuanza ufuaji wa
          FOR ONLINE READING ONLY
              chuma ili kupata mazao bora ya chuma na kulinda afya zao.
              Pia, uzalishaji wa chuma ulifanywa mbali kabisa na makazi ya

              jamii hasa porini ili kuzuia watu kuvuta hewa chafu yenye moshi
              uliotokana na fukuto wakati wa uyeyushaji wa chuma. Ufuaji wa
              chuma ulifanyika katika tanuru ili kuzuia athari za moto mkali
              kwa binadamu. Wanaume ndiyo waliohusika zaidi katika ufuaji
              wa chuma. Hii ilitokana na imani za jamii katika upatikanaji wa

              chuma na sababu za kiafya za afya ya uzazi kwa wanawake.

              Sayansi na teknolojia ya chuma na maendeleo ya uchumi
              na jamii

              Sayansi na teknolojia asili ya chuma ilileta mapinduzi makubwa
              katika sekta za uzalishaji mali na ulinzi katika jamii kabla ya

              ukoloni nchini. Kwa mfano, majembe yaliboresha kilimo na
              kuongeza uzalishaji katika kilimo. Binadamu alipanua mashamba
              ya kilimo kwa kufyeka, kulima na kupanda mazao katika maeneo
              makubwa zaidi. Upanuzi wa kilimo ulichangia kupatikana kwa

              chakula na ziada. Upatikanaji wa chakula uliboresha afya ya
              jamii, hali iliyoongeza afya ya uzazi na kusababisha ongezeko
              la watu. Hivyo, kuimarika kwa shughuli za uchumi katika jamii.
              Pia, afya bora ilisaidia kupunguza vifo vilivyotokana na lishe

              duni. Ongezeko la watu lilisababisha uhitaji wa uongozi na watu
              wenye mamlaka za uongozi katika jamii.


              Utengenezaji wa zana za uvuvi kama vile ndoano ulisaidia
              kuongeza mazao ya uvuvi. Utengenezaji wa vichwa vya mikuki
              na mishale kwa kutumia chuma, kuliboresha shughuli za uwindaji
              na zana za vita katika jamii. Aidha, sayansi na teknolojia ya
              asili katika chuma ilisababisha kuibuka kwa mafundi sanifu

              waliojulikana kama wahunzi. Wahunzi shughuli yao rasmi ilikuwa


                                                   54




                                                                                          06/11/2024   11:29:54
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   54                                     06/11/2024   11:29:54
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   54
   56   57   58   59   60   61   62   63   64   65   66