Page 66 - Historiayatznamaadili
P. 66

Jamii zilizojihusisha zaidi na ufugaji ni Wamasai, Wadatoga,
              Wajaluo, Wasukuma, Wairaqw na Wagorowa. Ufugaji ulifanyika
              kwa kupeleka wanyama katika malisho mbali na makazi ya watu.

              Mifugo iliwekwa katika maboma ambayo yalijengwa kwa kutumia
          FOR ONLINE READING ONLY
              nyasi, fito na matawi ya miba. Hii ilisaidia maboma haya kuwa

              na hewa ya kutosha na mifugo kuwa na ulinzi dhidi ya magonjwa
              na wanyama wakali.


              Sayansi na teknolojia za asili zilitumika ili kufahamu majira ya
              mwaka na viashirio vya ukame. Maarifa yalihusisha matumizi
              ya mwezi na pepo. Hii ilisaidia wafugaji kupata malisho na maji

              ya kutosha. Baadhi ya maeneo, wafugaji walijenga mabwawa
              ili kukusanya maji ya mvua kwa ajili ya matumizi ya baadaye.

              Maeneo yasiyo na maji ya kutosha, walichimba visima vifupi ili
              kupata maji.


              Pia, walitumia maarifa asilia kujua tabia za wanyama na afya
              zao. Mifugo ilitibiwa kwa kutumia mitishamba (dawa za asili).
              Mbinu mbalimbali za kiasili zilitumika wakati wa kuchunga

              mifugo. Mfano, mbwa waliofunzwa walitumika kuongoza
              mifugo. Pia, miluzi ilitumika kuongoza mifugo na kuwasiliana na

              wafugaji wengine. Palikuwako na aina tofauti za miluzi ambayo
              iliwezesha wafugaji kutambua ishara mbalimbali, mfano vizuizi
              dhidi ya wanyama wakali na kuwasiliana kwa kawaida. Mifugo

              ilivikwa kengele kwa ajili ya ulinzi dhidi ya wanyama wakali.
              Vilevile, sayansi na teknolojia za asili zilitumika katika uhifadhi

              wa mazao ya mifugo. Mfano, maziwa yaliwekwa kwenye vibuyu
              vya asili bila kuharibika. Miti maalumu ilitumika kusafishia vibuyu
              vya kuhifadhia maziwa ili kuzuia yasiharibike. Pia, sayansi na

              teknolojia asilia zilitumika kutengeneza samli kutoka katika
              maziwa ya ng’ombe.






                                                   59




                                                                                          06/11/2024   11:29:55
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   59
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   59                                     06/11/2024   11:29:55
   61   62   63   64   65   66   67   68   69   70   71