Page 45 - Historiayatznamaadili
P. 45

Baadhi ya jamii mpaka sasa bado zinaishi katika nyumba hizo.
              Tofauti ya nyumba za asili na za kisasa, ni kuwa nyumba za
              asili huwa na hewa safi na hazihifadhi joto kama ilivyo kwa
              nyumba za kisasa. Aidha, ni rahisi kuzijenga na hazina gharama
          FOR ONLINE READING ONLY
              kubwa katika ujenzi. Tofauti za makazi kwa sasa zimetokana na
              mwingiliano wa jamii. Hivyo, jamii zetu kuiga muundo wa ujenzi
              wa makazi ya sasa.

                                Kazi ya kufanya namba 12

                         Tembelea eneo la karibu lenye makazi ya nyumba za
                         asili kisha:

                         1.  Andika aina ya nyumba hizo na malighafi zilizotumika
                             katika ujenzi.

                         2.  Chora picha ya nyumba ya msonge, banda na
                             tembe.

                         3.  Andika mambo ya kujivunia kutokana na nyumba
                             za asili.

                         4.  Andika mambo ya kujifunza kuhusu makazi ya asili.





              Maendeleo ya jamii katika afya kabla ya ukoloni

              Afya ni hali ya kuwa mkamilifu kimwili na kiakili. Kwa maana
              nyingine, ni hali ya kutokuwapo kwa maradhi katika mwili wa
              binadamu au kuugua. Jamii yenye afya inaweza kushiriki katika
              shughuli za maendeleo binafsi, jamii na Taifa kwa jumla. Afya
              bora husaidia kuleta maisha bora na kupunguza umaskini.


                                Kazi ya kufanya namba 13


                            Waulize wazazi au walezi kuhusu mambo
                            yaliyozingatiwa katika afya ya jamii yako hapo kale.









                                                   38




                                                                                          06/11/2024   11:29:48
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   38
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   38                                     06/11/2024   11:29:48
   40   41   42   43   44   45   46   47   48   49   50