Page 36 - Historiayatznamaadili
P. 36

Pia, njia za masimulizi ya hadithi zilitumika kutoa mafunzo.
              Watu wenye umri mkubwa hasa wazee, walifundisha vijana
              na watoto maarifa na stadi za jamii inayohusika kwa njia ya
              masimulizi.  Hadithi  zilizosimuliwa zilijaa mafundisho yenye
              maadili, maarifa na ujuzi wa jamii. Hadithi hizo zilitumia maneno
          FOR ONLINE READING ONLY
              yenye mafumbo ili kufikirisha na kutoa mafunzo. Licha ya hadithi
              kutumika kufundisha maarifa na ujuzi wa asili wa jamii, zilisaidia
              watoto na vijana kujifunza utu, miiko, maadili na imani za jamii
              zao. Vilevile, hadithi zilisaidia kujifunza majukumu muhimu ya
              kiraia kwa mujibu wa mila na desturi za jamii inayohusika. Aidha,
              hadithi zilisadia vijana kujifunza shughuli za uzalishaji mali.

              Mbali na hadithi, palikuwapo na misemo, vitendawili na methali
              vilivyotumiwa kusisitiza maadili na kanuni za jamii.

              Baadhi ya maeneo yenye majabali na mapango makubwa
              yalitumika kama sehemu za kujifunzia. Mababu zetu walichora
              picha mbalimbali mapangoni ili kutoa elimu kuhusu mazingira,
              wanyama na wadudu wakali. Pia, picha hizo zilieleza namna ya
              kujenga jamii yenye amani, utulivu na kupenda kufanya kazi.
              Baadhi ya ushahidi wa picha hizo, ni michoro ya mapangoni
              iliyopo maeneo mbalimbali katika nchi yetu. Mfano, michoro
              ya mapangoni iliyopo katika Kata ya Kolo, Wilaya ya Kondoa,
              Mkoa wa Dodoma.


              Elimu ilitolewa kwa lugha zilizotumiwa kwa mawasiliano katika
              jamii inayohusika. Kwa mfano, Wagogo walijifunza kwa lugha
              ya Kigogo na Wasukuma kwa lugha ya Kisukuma na kadhalika.
              Hii ilisaidia kuwawezesha watoto kuelewa kwa urahisi mafunzo
              yaliyotolewa. Njia hii ya utoaji wa elimu, ilisaidia jamii kufahamu
              matarajio ya familia zao na shughuli za uchumi na jamii zao. Pia,
              ilisaidia kufahamu maarifa na ujuzi wa asili wa jamii zao kwa
              urahisi. Ingawa hapakuwa na mitihani kama ilivyo katika elimu
              ya sasa, mwanafunzi alipimwa kutokana na utendaji wake katika
              kazi. Pale mtoto alipoonekana kutokufikia vigezo vya ujifunzaji,
              alifundishwa zaidi ili aweze kufikia vigezo vilivyohusika. Msingi

              wa elimu yetu ya sasa nchini “Elimu ya Kujitegemea” imejengwa
              kutokana na elimu ya kabla ya ukoloni.


                                                   29




                                                                                          06/11/2024   11:29:40
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   29                                     06/11/2024   11:29:40
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   29
   31   32   33   34   35   36   37   38   39   40   41