Page 23 - Historiayatznamaadili
P. 23

Kuwaheshimu viongozi wa serikali
              Mtoto ana wajibu wa kuwaheshimu viongozi wa serikali katika
              ngazi zote za uongozi. Hii ni kuanzia ngazi za Mtaa/Kijiji, Kata,
              Wilaya, Mkoa na Taifa. Mtoto ana wajibu wa kuwaheshimu,
          FOR ONLINE READING ONLY
              kushirikiana nao na kuwatii katika matendo yaliyo mema ili
              kuwezesha utekelezaji wa kazi za ustawi wa jamii na Taifa zima.
              Heshima kwa viongozi, humsaidia mtoto kupata msaada na
              haki zake.


                      Zoezi namba 3

                1.  Eleza umuhimu wa mtoto kuheshimu na kushirikiana na
                      viongozi wa serikali katika matendo yaliyo mema.

                2.  Orodhesha matendo yanayoashiria mtoto kujilinda na
                      kujijali.


              Kupinga vitendo dhidi ya rushwa

              Mtoto anao wajibu wa kupinga vitendo vya rushwa kwani
              vinadhoofisha maendeleo ya jamii na Taifa. Vitendo vya rushwa

              huwanyima watu kupata haki na huduma bora katika jamii na
              Taifa.  Pia, husababisha ufujaji na ubadhilifu wa rasilimali za
              umma. Hivyo, mtoto ana wajibu wa kupinga vitendo vya rushwa
              na kushiriki kwa vitendo kulinda rasilimali za umma. Hii ni pamoja

              na kutoa taarifa za matumizi mabaya ya rasilimali za umma na
              kutumia vizuri miradi ya maendeleo kama vile miundombinu
              ya reli, barabara, majengo ya shule, miradi ya maji, visima,
              mabomba na vinginevyo katika jamii inayomzunguka. Pia, wajibu
              huu, unaweza kutekelezwa kwa kutoa elimu ya namna ya kuzuia
              na kupambana na rushwa na madhara ya rushwa. Mfano, kutoa
              elimu kupitia nyimbo, ngonjera, vipindi maalumu katika redio,

              runinga na matamasha ya kitaifa. Vilevile, mtoto ana wajibu wa
              kutoa taarifa katika Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa
              (TAKUKURU) akigundua vitendo vya rushwa katika jamii yake.
              Kielelezo namba 7, kinaonesha watoto wenye mabango ya
              kupinga vitendo vya rushwa.



                                                   16




                                                                                          06/11/2024   11:29:34
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   16
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   16                                     06/11/2024   11:29:34
   18   19   20   21   22   23   24   25   26   27   28