Page 21 - Historiayatznamaadili
P. 21

Kazi ya kufanya namba 13


                             Jadili namna ambavyo mtoto anaweza kulinda,
                             kuhifadhi na kudumisha uhuru na umoja wa Taifa.
          FOR ONLINE READING ONLY


              Mtoto anaweza kulinda, kuhifadhi na kudumisha uhuru na umoja
              wa jamii na Taifa kwa kuonesha upendo kwa watu wengine,
              kushirikiana na kuthamini utu wa binadamu wenzake.

              Kulinda usalama na amani ya jamii na Taifa

              Pamoja na Taifa kuwa na vyombo vya kusimamia usalama
              wa raia na mali zao, mtoto ana wajibu wa kulinda usalama na
              amani ya jamii na Taifa lake. Wajibu huu humpa mtoto nafasi
              ya uwajibikaji katika ulinzi na usalama wa jamii na Taifa lake.


                                Kazi ya kufanya namba 14

                             Jadili namna mtoto anavyoweza kushiriki katika
                             kulinda usalama na amani ya jamii na Taifa.




              Mtoto ana wajibu wa kutoa taarifa kwenye ofisi za Mtaa/Kijiji au
              polisi, iwapo ataona mazingira hatarishi ya uvunjaji wa sheria
              na kanuni za jamii au nchi ili kulinda usalama na amani ya jamii
              na Taifa lake. Pia, ni wajibu wa mtoto kutoa taarifa za vitendo
              viovu kama vile wizi, ugomvi, udhalilishaji, ukatili na unyanyasaji.


              Kujifunza utamaduni wa jamii na Taifa

              Mtoto ana wajibu wa kujifunza mambo mema ya utamaduni
              wa jamii na Taifa lake. Jamii ina mila na desturi zinazoongoza
              wanajamii ili kuishi kulingana na mahitaji yao. Mila na desturi
              hizi hueleza namna jamii inavyopaswa kuishi, kushirikiana na
              kuhusiana. Pia, huelezea mienendo ya jamii kiimani, kielimu,
              kimaadili na maarifa na ujuzi wa jamii inayohusika. Vilevile,
              hueleza malezi, tabia njema na jinsi ya kujifunza. Kwa ujumla,
              mila na desturi hubeba utambulisho wa jamii, ambao hutofautisha



                                                   14




                                                                                          06/11/2024   11:29:33
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   14
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   14                                     06/11/2024   11:29:33
   16   17   18   19   20   21   22   23   24   25   26