Page 13 - Historiayatznamaadili
P. 13

Kutokubaguliwa kwa njia yoyote
              Mtoto ana haki ya kutobaguliwa kwa njia yoyote iwe kwa rangi,
              jinsi, hali ya maisha, dini au hali itakayomfanya kuwa dhaifu na

              duni. Mtoto ana haki ya kutambua ndugu na jamaa zake katika
          FOR ONLINE READING ONLY
              familia, ukoo na jamii inayohusika.  Haki hii kimsingi inazuia
              mtoto kubaguliwa na kutoa nafasi kwake ya kupata huduma za
              kijamii na kisheria ili kumlinda dhidi ya ubaguzi na unyanyasaji
              katika jamii inayomzunguka.


                      Zoezi namba 1


                1.  Eleza matendo yanayoashiria kubaguliwa kwa mtoto.

                2.  Ainisha huduma anazostahili kupata mtoto katika jamii
                      na Taifa kwa ujumla.





              Kupata hifadhi ya maisha katika jamii na Taifa

              Mtoto ana haki ya kuishi kama mtu huru katika jamii na Taifa.
              Haki hii inakataza mtoto kufungiwa ndani, kuhamishwa kwa
              nguvu, au kunyang’anywa kwa nguvu uhuru wake kutoka katika
              familia, jamii au Taifa lake. Aidha, mtoto anaweza kupata hifadhi
              sehemu nyingine nje ya familia yake pale itakapothibitika kuwa
              anateseka akiwa ndani ya familia yake.


              Haki ya kujua utamaduni wa jamii na Taifa lake

              Mtoto ana haki ya kujua utamaduni wa jamii na Taifa lake.
              Haki hii humpa mtoto nafasi ya kufahamu lugha ya jamii yake,

              vyakula, mavazi na michezo katika jamii na Taifa lake.  Pia,
              humpa mtoto nafasi ya kutambua miiko na imani za jamii yake.
              Utambuzi wa utamaduni humpa mtoto nafasi ya kujua matendo
              yanayokubalika na yasiyokubalika katika jamii na Taifa lake.
              Vilevile, humpa mtoto nafasi ya kupata elimu ya malezi na
              makuzi bora yanayoendana na mila na desturi za jamii na Taifa
              kwa ujumla.



                                                    6




                                                                                          06/11/2024   11:29:28
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   6
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   6                                      06/11/2024   11:29:28
   8   9   10   11   12   13   14   15   16   17   18