Page 11 - Historiayatznamaadili
P. 11

FOR ONLINE READING ONLY




























                    Kielelezo namba 2: Watoto wakiwa darasani wakipata elimu
              Serikali imeweka programu za kutoa elimu bila malipo katika
              shule zinazomilikiwa na serikali nchini kote. Pia, imeimarisha
              miundombinu katika shule hizo, na kutoa vifaa vya kufundishia
              na kujifunzia ili kuwapatia watoto elimu kama haki yao ya msingi.
              Hii inafanyika ili kuweka fursa sawa ya kupata elimu kwa kila

              mtoto ambayo ni haki stahiki.  Haki ya elimu huwezesha kila
              mtoto kupata maarifa na ujuzi utakaomwezesha kuchangia
              katika maendeleo yake, ya jamii na Taifa kwa ujumla.


              Kuheshimiwa, kutambuliwa na kuthaminiwa utu wake
              Mtoto ana haki ya kuheshimiwa, kutambuliwa na kuthaminiwa

              utu wake. Hii ni pamoja na kutohusishwa katika aina yoyote ya
              udhalilishaji utakaomvunjia heshima mtoto. Haki hii ni ya msingi
              ili kumpa mtoto haki ya faragha na usalama dhidi ya vitendo vya
              ukatili, uonevu, unyanyasaji na udhalilishaji.





                                                    4




                                                                                          06/11/2024   11:29:27
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   4
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   4                                      06/11/2024   11:29:27
   6   7   8   9   10   11   12   13   14   15   16