Page 10 - Historiayatznamaadili
P. 10

2019. Haki hizo zinatambuliwa kisheria na inakatazwa mtu au
              mamlaka yoyote kukiuka haki hizo katika jamii na Taifa. Uwapo
              wa haki hizo, unatoa nafasi kwa mtoto kulindwa dhidi ya ukiukwaji
              wa haki za mtoto kunakoweza kusababisha unyanyasaji, ukatili
          FOR ONLINE READING ONLY
              na udhalilishaji wa mtoto. Mtoto si wa familia peke yake, bali ni
              mali ya jamii na Taifa kwa ujumla, ndiyo maana haki za mtoto,
              zimetafsiriwa katika ngazi ya jamii na Taifa. Kielelezo namba 1,
              kinaonesha baadhi ya haki za mtoto katika jamii na Taifa.



































                       Kielelezo namba 1: Haki za mtoto katika jamii na Taifa

              Kupata elimu na kujielimisha

              Familia inajukumu la msingi la kumpa mtoto elimu. Aidha, jamii
              na Taifa wana wajibu wa kumwendeleza mtoto kwa kumpa elimu.
              Hii ni pamoja na kumpa elimu ya mila na desturi za jamii na Taifa.
              Pia, haki hii humpa mtoto nafasi ya kupata habari na elimu ya
              kutosha ili aweze kujitambua na kuchangia katika maendeleo

              ya jamii na Taifa. Aidha, mtoto ana wajibu wa kusoma kwa bidii
              ili kupata elimu iliyokusudiwa. Kielelezo namba 2, kinaonesha
              watoto wakiwa darasani wakipata elimu.



                                                    3




                                                                                          06/11/2024   11:29:26
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   3
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   3                                      06/11/2024   11:29:26
   5   6   7   8   9   10   11   12   13   14   15