Page 9 - Historiayatznamaadili
P. 9

hata ambao siyo Watanzania lakini wanaishi Tanzania. Vilevile,
              kuna sheria zinazofafanua wajibu wa mtu mzima na watoto.
              Wajibu huo umezingatia umri, jinsi, na madaraka ili kurahisisha
              utekelezaji wake kulingana na matarajio ya jamii na Taifa. Hivyo,
              mtu asipotimiza wajibu fulani, anawajibishwa na kuadhibiwa kwa
          FOR ONLINE READING ONLY
              mujibu wa sheria zinazohusika.


              Haki hutofautiana na wajibu. Haki hujumuisha matendo au
              vitu vya msingi ambavyo mtu anastahili kupata na kutendewa
              katika jamii inayohusika. Mtoto huzaliwa na hulelewa katika
              jamii, ambayo hujumuisha familia, ukoo, kabila, Kijiji/Mtaa, Kata,
              Tarafa na Taifa. Mazingira haya ni msingi wa mtoto kupata haki
              zake. Aidha, kutokana na msisitizo wa haki za binadamu, haki
              za mtoto zimewekwa kisheria zikieleza ni kipi ambacho mtu

              mzima, jamii na Taifa hupaswa kutimiza kwa mtoto kama haki
              zake.  Haki hizo zinalenga kueleza namna jamii inavyopaswa
              kumpa mtoto ulinzi, mahitaji muhimu na nafasi za ushiriki katika
              kujenga jamii na Taifa. Kimsingi, mahitaji ya mtoto ndiyo hutafsiri
              haki za mtoto kuanzia katika ngazi ya familia, jamii na Taifa.


              Haki za mtoto katika jamii na Taifa

                                Kazi ya kufanya namba 2


                           Jadili haki za mtoto katika jamii na Taifa kama
                           zilivyotafsiriwa katika sheria ya mtoto, sura ya 13
                           ya mwaka 2009 na katiba ya Jamhuri ya Muungano

                           wa Tanzania ya mwaka 1977.


              Haki za mtoto zimetafsiriwa kwa mujibu wa sheria, kanuni na
              taratibu za serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na
              mataifa mbalimbali. Kwa mfano, Katiba ya Jamhuri ya Muungano
              wa Tanzania ya mwaka 1977, Sura ya Kwanza, Sehemu ya Tatu,
              Ibara ya 12-24, inaeleza kuhusu haki za binadamu akiwamo
              mtoto katika jamii na Taifa. Pia, haki za mtoto zimeelezwa katika
              sheria ya mtoto, Sura ya 13 ya Mwaka 2009, toleo la mwaka




                                                    2




                                                                                          06/11/2024   11:29:25
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   2                                      06/11/2024   11:29:25
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   2
   4   5   6   7   8   9   10   11   12   13   14