Page 14 - Historiayatznamaadili
P. 14

Kazi ya kufanya namba 5


                           Jadili  umuhimu wa  mtoto  kutambua  utamaduni
                           wa jamii na Taifa lake wakati huu wa usasa na
          FOR ONLINE READING ONLY
                           utandawazi.

              Haki hizi za mtoto zinapaswa kulindwa na watu wote kuanzia
              katika ngazi ya familia, jamii na Taifa.  Aidha, serikali kwa
              kutambua hilo, imeweka maofisa wanaosimamia utekelezaji wa
              haki za mtoto katika ngazi za Mitaa, Vijiji, Kata, Wilaya, Mikoa
              na Taifa. Pia, vituo vya usalama, mfano polisi vina dawati la
              masuala ya jinsia na ulinzi wa watoto. Dawati hili husimamia
              utekelezaji wa haki za mtoto. Vilevile, ofisi za Kata na Mtaa/Kijiji
              zina maofisa wanaosimamia haki za watoto. Aidha, viongozi wa
              asasi za kidini husimamia utekelezaji wa haki za mtoto katika
              jamii na Taifa.  Walimu katika ngazi zote za elimu wana wajibu
              wa kulinda na kusimamia haki za mtoto. Watu hawa wote wana
              wajibu wa kusimamia ulinzi na usalama wa mtoto ili kuhakikisha
              haki za mtoto zinalindwa ipasavyo. Hivyo, kuwezesha katika

              ukuaji wa mtoto kiakili, kimwili, kisaikolojia, kimaono na kiroho.

                                Kazi ya kufanya namba 6


                           Jadili changamoto zinazoweza kuwakabili watoto
                           katika upatikanaji wa haki zao na jinsi ya kuzitatua
                           katika jamii inayokuzunguka.



              Wajibu wa mtoto katika jamii na Taifa
              Sheria ya mtoto ya mwaka 2009, toleo la mwaka 2019 imeeleza
              wazi wajibu wa mtoto katika jamii na Taifa lake.

                                Kazi ya kufanya namba 7


                           Jadili wajibu wa mtoto katika jamii na Taifa kama
                           ilivyotafsiriwa katika sheria ya mtoto ya mwaka
                           2009, toleo la mwaka 2019 na Katiba ya Jamhuri
                           ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977.



                                                    7




                                                                                          06/11/2024   11:29:28
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   7
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   7                                      06/11/2024   11:29:28
   9   10   11   12   13   14   15   16   17   18   19