Page 6 - SayansiStd4
P. 6

Utangulizi

              Kitabu cha Sayansi kimetayarishwa kwa kuzingatia muhtasari
              wa somo la Sayansi Elimu ya Msingi Darasa la III-VI uliotolewa

              na Wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia mwaka 2023. Baadhi
          FOR ONLINE READING ONLY
              ya maudhui ya kitabu hiki yamechukuliwa kutoka katika vitabu
              vya Sayansi  na  Teknolojia  Darasa  la  Tatu, Nne,  Tano, Sita
              na Saba. Vitabu hivyo vilichapishwa mwaka 2018 na Darasa
              la Saba mwaka 2021 kwa kuzingatia muhtasari wa Somo la

              Sayansi na Teknolojia wa mwaka 2016. Kitabu hiki kina sura
              sita ambazo ni Kanuni za afya, Magonjwa, Maada, Uunguaji
              wa vitu, Nishati na Usimbaji katika kompyuta.


              Maudhui ya kitabu hiki yamewasilishwa kwa njia ya matini, kazi
              za kufanya, majaribio, mazoezi, michoro na picha mbalimbali
              ili kukuwezesha kujenga umahiri uliokusudiwa katika kila

              sura. Kila sura ina kazi za kufanya na mazoezi ya kutosha
              yatakayokuwezesha  kupima uelewa  wako kuhusu maudhui
              husika. Unatakiwa kufanya kazi zote, majaribio,  maswali  na
              mazoezi peke yako au kwa kushirikiana na wenzako.


              Aidha, unashauriwa kuwashirikisha walimu, wazazi au walezi
              unapotumia  maktaba, mtandao au vyanzo vingine kutafuta

              taarifa. Jifunze zaidi kupitia maktaba mtandao
              https://ol.tie.go.tz au ol.tie.go.tz
















                                                          Taasisi ya Elimu Tanzania





                                                    v




                                                                                            14/01/2025   18:38
     SAYANSI DARASA LA IV KITABU CHA MWANAFUNZI.indd   5
     SAYANSI DARASA LA IV KITABU CHA MWANAFUNZI.indd   5                                    14/01/2025   18:38
   1   2   3   4   5   6   7   8   9   10   11