Page 9 - SayansiStd4
P. 9

FOR ONLINE READING ONLY









                (a)  Kufanya mazoezi ya mwili                  (b)  Kula mlo kamili

                            Kielelezo namba 1: Kuzingatia kanuni za afya




                Kazi ya kufanya namba 1


               Tumia maktaba, matini mtandao au vyanzo vingine vya taarifa

               kutafuta taarifa kuhusu kanuni za afya. Wasilisha taarifa hizo
               darasani kwa ajili ya majadiliano.



              Mlo kamili

              Mlo kamili ni mlo wenye virutubisho vyote vya chakula katika

              uwiano sahihi. Mlo kamili huundwa na vyakula kutoka katika
              makundi makuu matatu. Mosi ni vyakula vya kuupa mwili nguvu.
              Vyakula hivyo vina virutubisho vya kabohaidreti au wanga. Pili,

              ni vyakula vya kujenga mwili vyenye virutubisho vya protini.
              Mwisho ni vyakula  vya kulinda mwili vyenye virutubisho vya

              vitamini na madini. Mlo kamili hutupatia virutubisho vyote muhimu
              ambavyo mwili unahitaji kwa uwiano sahihi. Umuhimu wa mlo
              kamili ni kuimarisha kinga ya mwili ili kuweza kupambana na

              magonjwa. Kielelezo namba 2 kinaonesha mfano wa makundi
              makuu ya vyakula katika mlo kamili.







                                                    2



                                                                                            14/01/2025   18:38
     SAYANSI DARASA LA IV KITABU CHA MWANAFUNZI.indd   2
     SAYANSI DARASA LA IV KITABU CHA MWANAFUNZI.indd   2                                    14/01/2025   18:38
   4   5   6   7   8   9   10   11   12   13   14