Page 12 - SayansiStd4
P. 12

misuli na mifupa ya mwili.Vitamini na madini  hupatikana
              katika mbogamboga kama vile kabichi, sukumawiki, mchicha,
              biringanya  na karoti.  Pia,  hupatikana katika  matunda mfano
              papai, chungwa, parachichi, zabibu na embe. Kielelezo namba
          FOR ONLINE READING ONLY
              5 kinaonesha mifano ya vyakula vyenye vitamini na madini.






















                       Kielelezo namba 5: Vyakula vyenye vitamini na madini

              Maji

              Maji  si sehemu  ya makundi  makuu  ya vyakula  yanayounda

              mlo kamili. Hatahivyo, mwili huhitaji  maji ya kutosha ili
              uweze kufanya kazi ipasavyo. Hii ni kwa sababu yana madini
              mbalimbali yanayosaidia mifumo ya mwili kufanya kazi vizuri.
              Kwa mfano, umeng’enywaji wa chakula na ufyonzwaji mzuri wa

              virutubisho kutoka kwenye vyakula. Pia, maji husaidia kuondoa
              takamwili na sumu mwilini. Vilevile, maji husaidia kurekebisha
              joto la mwili.



                Kazi ya kufanya namba 3


               1.  Pangilia mlo kamili wa mchana kwa kutumia vyakula
                     vinavyopatikana katika maeneo yako.


               2.  Eleza umuhimu wa kila aina ya chakula iliyojumuishwa
                      kwenye mlo wako.



                                                    5




                                                                                            14/01/2025   18:38
     SAYANSI DARASA LA IV KITABU CHA MWANAFUNZI.indd   5
     SAYANSI DARASA LA IV KITABU CHA MWANAFUNZI.indd   5                                    14/01/2025   18:38
   7   8   9   10   11   12   13   14   15   16   17