Page 14 - SayansiStd4
P. 14

Vijanabalehe

              Hili ni kundi lililopo  katika kipindi  cha balehe. Katika kipindi
              hiki mwili hupitia  mabadiliko  na  kukua kwa haraka, hivyo
              kijana huhitaji mlo wenye vyakula vya  kutosha vya  kujenga,
          FOR ONLINE READING ONLY
              kulinda na kuupa mwili nguvu na joto. Katika umri huu, kijana

              hujishughulisha  na shughuli  mbalimbali  kama vile  michezo,
              kulima au kusoma kwa muda mrefu. Hivyo, ni muhimu mlo wa
              kijana uwe na kiwango kikubwa cha vyakula vya kuupa mwili
              nguvu. Hii ni kwa sababu  mwili unahitaji nguvu za kutosha

              kuzimudu shughuli zake. Kielelezo namba 7 kinaonesha mlo
              kamili wa kijanabalehe.



                                                                          Vyakula vya
                                                                          kuupa mwili

                 Vyakula                                                  nguvu
                 vya kujenga
                 mwili












                                                                        Vyakula vya
                                                                        kulinda mwili



                           Kielelezo namba 7: Mlo kamili wa kijanabalehe


              Wazee

              Kinga  ya mwili  hupungua  katika kipindi  cha uzee. Hivyo,
              wazee wanatakiwa kula vyakula vyenye vitamini ili kujikinga na
              magonjwa ya mara kwa mara. Pia, wanapaswa kula vyakula
              vyenye madini mbalimbali ili kuimarisha mifupa,  na misuli ya

              mwili. Vilevile, wanatakiwa kula kiasi kidogo cha vyakula vya


                                                    7




                                                                                            14/01/2025   18:38
     SAYANSI DARASA LA IV KITABU CHA MWANAFUNZI.indd   7                                    14/01/2025   18:38
     SAYANSI DARASA LA IV KITABU CHA MWANAFUNZI.indd   7
   9   10   11   12   13   14   15   16   17   18   19