Page 19 - SayansiStd4
P. 19

Faida za kufanya mazoezi ya mwili

              Inashauriwa kufanya mazoezi ya mwili mara kwa mara. Kufanya
              mazoezi ya mwili mara kwa mara husaidia yafuatayo:

          FOR ONLINE READING ONLY
              (a)  Kuwa na afya bora;

              (b)  Kurekebisha utendaji wa mifumo ya mwili kama vile mfumo
                   wa mzunguko wa damu, mmeng’enyo wa chakula na utoaji
                   takamwili;


              (c)  Kuimarisha  kinga  ya mwili  ili  kupambana  na magonjwa
                   mbalimbali;

              (d)  Kuondoa msongo wa mawazo na sonona; na

              (e)  Kuchangamsha ubongo na kuburudika.


              Madhara ya kutofanya mazoezi ya mwili

              Kutofanya mazoezi ya mwili husababisha madhara yafuatayo:

              (a)  Kuwa na afya duni na dhaifu;


              (b)  Uzito wa mwili unaweza kuongezeka kupita kiasi, hivyo
                   kuwa kwenye hatari ya kupata kiribatumbo;

              (c)  Kupata magonjwa  yanayoambatana  na uzito mkubwa

                   kama vile shinikizo la damu, kisukari na matatizo ya moyo;

              (d)  Kupata msongo wa mawazo na sonona; na

              (e)  Udhaifu wa misuli na mifupa.


              Usafi wa mwili na mazingira
              Usafi wa mwili na mazingira ni muhimu ili kuwa na afya bora.

              Miili  yetu  inapaswa  kuwa  safi  wakati  wote.  Pia,  mavazi  na
              maeneo yanayotuzunguka yanapaswa kuwa safi kwa wakati
              wote.







                                                   12



                                                                                            14/01/2025   18:38
     SAYANSI DARASA LA IV KITABU CHA MWANAFUNZI.indd   12
     SAYANSI DARASA LA IV KITABU CHA MWANAFUNZI.indd   12                                   14/01/2025   18:38
   14   15   16   17   18   19   20   21   22   23   24