Page 21 - SayansiStd4
P. 21

Baada ya kuoga, kausha mwili kwa taulo safi. Pia, paka mafuta
              mwilini baada ya kuoga ili kuepuka ngozi kuwa kavu.




          FOR ONLINE READING ONLY
                Kazi ya kufanya namba 7


               1.  Tumia maktaba, matini mtandao  au vyanzo vingine
                     kutafuta taarifa kuhusu vifaa na hatua za kuoga.


               2.  Wasilisha  taarifa ulizozitafuta, darasani  kwa ajili  ya
                     majadiliano.




              Usafi wa nywele

              Nywele zinatunzwa kwa kuziosha mara kwa mara kwa kutumia
              maji safi na sabuni. Vilevile, kwa kusuka, kunyoa au kuchana ili
              zionekane safi na nadhifu. Nywele safi zinaepusha magonjwa

              ya ngozi ya kichwa kama vile mapunye na wadudu kama vile
              chawa.

              Usafi wa kucha


              Kucha za miguuni na mikononi zinatakiwa kuwa fupi ili kuepuka
              uchafu. Kucha ndefu zinahifadhi  uchafu unaoweza  kuwa
              na vimelea vya magonjwa.  Tunapaswa kuosha mikono na
              kusafisha kucha kwa maji safi na sabuni. Hii husaidia kuondoa
              uchafu na vijidudu vinavyosababisha magonjwa.


              Usafi wa nguo

              Nguo zinatakiwa kufuliwa  kwa maji safi na sabuni ili kuondoa
              uchafu. Nguo chafu  hufanya mwili kutoa harufu mbaya na

              zinaweza kuleta magonjwa ya ngozi kamavile muwasho na
              harara. Nguo iliyofuliwa inapaswa kukaushwa na kunyooshwa








                                                   14



                                                                                            14/01/2025   18:38
     SAYANSI DARASA LA IV KITABU CHA MWANAFUNZI.indd   14
     SAYANSI DARASA LA IV KITABU CHA MWANAFUNZI.indd   14                                   14/01/2025   18:38
   16   17   18   19   20   21   22   23   24   25   26