Page 25 - SayansiStd4
P. 25

Alama za kuzuia au kukataza

              Alama hizi zinatoa taarifa kuhusu jambo lisiloruhusiwa. Rangi
              ya alama hizi ni nyekundu. Pia, zina umbo la duara, picha nyeusi
              kwenye msingi mweupe na kingo nyekundu. Baadhi ya alama
          FOR ONLINE READING ONLY
              hizi zina mstari mwekundu wa kiegama. Mfano wa alama hizi ni

              kama vile huruhusiwi kuingia na huruhusiwi kula wala kunywa.
              Kielelezo namba 14 kinaonesha mifano ya alama za kuzuia au
              kukataza.















                                                               Hairuhusiwi kula wala
                    Hairuhusiwi kuingia                                kunywa
















                     Maji yasiyosalama                           Usitupe taka ovyo

                    Kielelezo namba 14: Mifano ya alama za kuzuia au kukataza


              Alama za dharura

              Alama hizi zinatoa maelekezo  ya kufanya jambo husika
              hususani dharura kama vile ajali. Alama hizo zinaonesha eneo
              la karibu lenye usalama au maelekezo ya kufikia eneo salama
              au vifaa vitakavyosaidia. Miongoni mwa alama hizo ni pamoja

              na simu za dharura na sanduku la huduma ya kwanza. Alama
              hizi zina rangi ya kijani. Pia, zina umbo la pembe nne, picha



                                                   18



                                                                                            14/01/2025   18:39
     SAYANSI DARASA LA IV KITABU CHA MWANAFUNZI.indd   18                                   14/01/2025   18:39
     SAYANSI DARASA LA IV KITABU CHA MWANAFUNZI.indd   18
   20   21   22   23   24   25   26   27   28   29   30