Page 109 - Historia_Maadili
P. 109

Faharasa



           Afrikanaizesheni      Utaratibu wa kuwaingiza na kuwapa Waafrika wenye sifa
                                 madaraka ya kiuchumi, kijamii na kisiasa baada ya nchi
                                 za Kiafrika kupata uhuru kutoka kwa wakoloni
        FOR ONLINE READING ONLY
           Bepari                Mtu ambaye  ni mfanyabiashara  na tajiri  mkubwa
                                 anayemiliki njia kuu za uzalishajimali kama vile viwanda
                                 na masoko

           Falsafa               Stadi ya maarifa, imani, maisha, chanzo chake na sababu
                                 za kuwapo kwake

           Itikadi               Imani au msimamo wa mtu au watu kuhusu jambo fulani
                                 mfano dini, chama, mawazo

           Kasumba               Fikra  za  mtu  zinazojengeka  kutokana  na  kuathiriwa
                                 kielimu,  kiutamaduni  au kiutawala  na jamii  fulani
                                 iliyomzunguka


           Kibaraka              Mtu mwenye uwezo wa chini kifedha na anayetumiwa
                                 na watu wengine kwa masilahi ya watu hao pasi na kujali
                                 madhara wanayopata watu wengine

           Propaganda            Taarifa  zisizo  na  ukweli  ambazo  hutumika  katika
                                 uhamasishaji wa watu ili wafuate mtazamo tofauti na ule
                                 waliokuwa nao

           Manamba               Mfanyakazi aliyetoka  mbali kwa ajili  ya kufanya kazi
                                 katika mashamba makubwa yaliyokuwa yanamilikiwa na
                                 watu wengine hasa walowezi

           Telegramu             Taarifa ya maandishi inayotumwa kwa njia ya simu

           Walowezi              Watu  wanaotoka  nchi  moja  na kuhamia  nchi  au eneo
                                 lingine  kwa nia  ya  kudhibiti,  kuendeleza,  au  kutumia
                                 rasilimali za eneo hilo.

           Wazawa                Watu ambao wamezaliwa na kukulia katika eneo au nchi
                                 fulani na ni wenyeji wa eneo hilo. Kwa mfano, “wazawa
                                 wa Tanzania”










                                                 101




                                                                                        03/10/2024   18:15:21
   HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd   101
   HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd   101                                        03/10/2024   18:15:21
   104   105   106   107   108   109   110   111   112