Page 106 - Historia_Maadili
P. 106

Vilevile, Mapinduzi ya Zanzibar yalichochea muungano kati ya Zanzibar na
          Tanganyika na hatimaye kuundwa kwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mwaka
          1964. Muungano huu uliwaleta pamoja watu kutoka asili na kanda mbalimbali.
          Hivyo, kuimarisha hisia ya utambulisho wa kitaifa na umoja. Sababu za kihistoria
          na kiuhusiano zilizosababisha kuungana kwa nchi hizi baada ya Mapinduzi zilifanya
          muungano huu ufanikiwe na kuendelea kudumu hadi leo. Pia, nia ya viongozi wa
        FOR ONLINE READING ONLY
          pande zote mbili, yaani Mwalimu Julius Kambarage Nyerere wa Tanganyika na
          Sheikh Abeid Amani Karume wa Zanzibar, ya kudumisha umoja na mshikamano wa
          kitaifa, hivyo ilichangia sana katika kufanikisha muungano huu.


          Kujenga mshikamano
          Mapinduzi ya Zanzibar yalichangia kwa kiasi kikubwa kuleta mshikamano wa
          kitaifa miongoni mwa wananchi. Hii ilifanikishwa kupitia kuundwa kwa serikali
          inayowakilisha makundi yote ya kijamii na kuondoa mgawanyiko wa kikabila na
          kidini. Maadili ya mshikamano, upendo na umoja yalikuzwa na hivyo yameendelea
          kuwa nguzo muhimu katika ujenzi wa taifa.

          Aidha, Serikali ya Mapinduzi Zanzibar ilipitisha kanuni za ujamaa na udugu ambazo
          zilisisitiza usawa, umiliki wa pamoja wa rasilimali na mshikamano. Huduma za jamii
          kama vile elimu, afya na makazi zilitolewa kwa usawa kwa wote bila kujali rangi,
          kabila, au dini ya mtu. Misingi hii iliendana na ile ya serikali ya Tanganyika na itikadi
          ya pamoja ilisaidia kuwaunganisha watu wa Zanzibar na Tanganyika chini ya dira
          ya pamoja ya kitaifa.


          Vilevile, Mapinduzi ya Zanzibar yalichochea hisia ya fahari ya kitaifa, uzalendo na
          kujitolea kwa manufaa ya wote, ambayo yameendelea kujenga mfumo wa maadili
          wa taifa hadi sasa. Mshikamano huu ulikuwa muhimu katika kuhamasisha wananchi
          kuunga mkono serikali mpya na sera zake. Serikali ya ASP ilifanya kazi ya kukuza
          mshikamano wa kijamii kwa kuzuia sera zote za kibaguzi na kuweka misingi thabiti
          ya usawa, utu, heshima na kuboresha hali ya maisha ya watu katika nyanja zote.



           Kazi ya kufanya 6.3


            Soma matini mbalimbali yanayohusu mapinduzi ya kisiasa katika nchi mbalimbali
            duniani, kisha eleza ni kwa namna gani mapinduzi yanavyoweza kujenga umoja
            na mshikamano kwa taifa linalohusika.







                                                  98




                                                                                        03/10/2024   18:15:20
   HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd   98                                         03/10/2024   18:15:20
   HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd   98
   101   102   103   104   105   106   107   108   109   110   111