Page 103 - Historia_Maadili
P. 103

Hata hivyo, Waafrika ndio walioathirika zaidi katika mfumo  wa kibaguzi wa kikoloni.
          Pamoja na wingi wao kufikia 85% ya watu wote wakati wa Mapinduzi, walipata
          huduma kidogo sana (chini ya 12%) ukilinganisha na wengine kama Waarabu na
          Wahindi. Wahindi na Waarabu ndio waliopata nafasi kubwa zaidi katika kupata
          huduma za kijamii, hasa maji, afya na elimu. Hivyo, ubaguzi katika nyanja mbalimbali
        FOR ONLINE READING ONLY
          ulileta chuki na kusababisha kuzuka kwa Mapinduzi ya Zanzibar mnamo Januari 1964.

          Sababu za kiuchumi: Kabla ya ujio wa Waarabu, kilimo na uvuvi vilikuwa shughuli
          kuu za kiuchumi kwa Wazanzibari. Wazanzibari walilima mazao ya chakula kama
          vile mihogo, ndizi, nazi na mtama kwa ajili ya chakula na biashara. Pia, jamii
          hizi zilijihusisha na shughuli za ufugaji na utengenezaji wa zana za kazi. Vilevile,
          mazingira ya visiwa yaliruhusu uvuvi, ambao ulikuwa sehemu muhimu ya maisha
          ya Wazanzibari. Jamii hizi zilitumia mitumbwi ya kienyeji, madema na nyavu za
          mikono katika shughuli za uvuvi, hususani uvuvi wa samaki.

          Hata hivyo, taratibu hizi zilibadilika mara baada ya kuja kwa wageni, yaani Waarabu

          na baadaye Wazungu wakati wa ukoloni. Wageni, hususani Waarabu walinyakua
          rasilimali kama vile ardhi nzuri kwa kilimo cha minazi na mikarafuu kwa manufaa yao
          binafsi na ya ukoloni. Wazanzibari wengi walinyang’anywa ardhi yao yenye rutuba
          na kubaki vibarua katika mashamba ya karafuu na minazi, pamoja na kufanya kazi
          za ndani. Wahindi walitawala biashara zote za jumla na rejareja madukani wakiwa
          pamoja na baadhi ya Waarabu. Hivyo, Mapinduzi ya mwaka 1964 yalikuwa ni ya
          lazima ili kupinga na kuondoa utawala dhalimu wa kikoloni, kulinda rasilimali za

          Wazanzibari na kujenga jamii inayozingatia misingi ya utu, usawa, haki na uwajibikaji
          kiuchumi.

          Chama cha ASP kilifanya mikutano ya hadhara na kutumia vyombo vya habari
          kufichua  maovu  na  unyanyasaji  uliofanywa  na  wakoloni.  Kwa  mfano,  mwezi
          Desemba 1959, katika viwanja vya Raha Leo, Sheikh Abeid Amani Karume alitangaza
          kwenye mkutano wa hadhara kwamba ASP ilitaka Zanzibar ipate uhuru na kuwa
          jamhuri. Serikali ya kikoloni haikukubaliana na kauli hiyo. Kwa kuwa milango yote

          ya kidemokrasia kwa Waafrika ilikuwa imefungwa, ASP iliona kuwa njia pekee ya
          kuleta uhuru wa kweli Zanzibar ni mapinduzi. Ndipo ilipofika tarehe 12 Januari 1964,
          ASP iliongoza Mapinduzi hayo na kuwakomboa Wazanzibari.










                                                  95




                                                                                        03/10/2024   18:15:19
   HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd   95                                         03/10/2024   18:15:19
   HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI F2.indd   95
   98   99   100   101   102   103   104   105   106   107   108